.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 31 Mei 2015

Tagged Under:

STARTIMES KUANZA KUONYESHA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA U20

By: Unknown On: Jumapili, Mei 31, 2015
  • Share The Gag

  • Na Dotto Mwaibale
    WAPENZI wa soka nchini sasa watafaidi kwa kutazama michuano ya kombe la dunia chini ya miaka 20 mwaka 2015 moja wa moja kwenye luninga zao kupitia ving’amuzi vya StarTimes pekee.
    Michuano hiyo ambayo itaanza kutimua vumbi tarehe 30 mwezi Mei na kumalizika tarehe 20 mwezi Juni mwaka huu moja kwa moja kutoka nchini New Zealand ambapo timu 24 za vijana kutoka mataifa mbalimbali duniani yatachuana kuwania ubingwa.
    Akizungumza baada ya kupata haki miliki kutoka kwa FIFA za kutangaza michuano hiyo maarufu duniani ambayo hubeba mastaa wa baadae kwa timu zao za taifa, Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif amesema kuwa wanafuraha kubwa kuonyesha michuano hiyo kwani soka ni mchezo unaopendwa zaidi duniani.
    “Tunayofuraha kubwa kuwatangazia wateja wetu kuwa tumepata haki miliki kutoka FIFA za kuonyesha michuano ya kombe la dunia kwa vijana wa umri chini ya miaka 20 mwaka 2015 itakayofanyika nchini New Zealand. Soka ni mchezo unaopendwa zaidi nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla na tunaamini tutawapatia wateja wetu burudani ya matangazo yenye ubora wa hali ya juu kupitia ving’amuzi vya StarTimes.” Alisema Bi. Hanif

    0 maoni:

    Chapisha Maoni