Norwich
City Leo hii wamefanikiwa kurudi tena Ligi Kuu England baada ya
kuporomoka Msimu mmoja uliopita baada ya kuichapa 2-0 Middlesbrough kwenye Fainali ya Mchujo wa Timu 4 za Daraja la Championship iliyochezwa Uwanjani Wembley Jijini London.
Mbele ya Watazamaji 85,656, Norwich City walipiga Bao zao 2 ndani ya Robo Saa ya Kwanza kwa Bao za Cameron Jerome alietumia vyema makosa ya Daniel Ayala na kufunga na kisha katika Dakika ya 15 Nathan Redmond alipiga Bao la Pili.
Norwich
City, ambao walimaliza Ligi ya Championship Nafasi ya 3 na hivyo kukosa
nafasi ya kupanda Ligi Kuu England moja kwa moja, kwenye Nusu Fainali
ya Mechi hizi za Mchujo waliibwaga Ipswich Town Jumla ya Mabao 4-2
katika Mechi mbili.
Boro walitinga Fainali hii kwa kuichapa Brentford Jumla ya Mabao 5-1 katika Mechi mbili. Norwich City sasa wameungana na Bournemouth na Watford, ambazo zilimaliza Nafasi mbili za juu za Ligi ya Championship na kupanda Daraja moja kwa moja, kucheza Ligi Kuu England Msimu ujao kuzibadili Hull City, QPR na Burnley zilizoporomoka Daraja.
Mashabiki wa Boro
Timu zikiingia Uwanjani Wembley
Kikosi cha Norwich
Kipute kimeanza ...mchezaji wa Boro chini
Jerome ndie aliyeanza kufunga bao la kwanza
Jerome akishangilia bao lake la kwanza
Meneja wa Noewich Alex Nail akishangilia nae
Nathan Redmond alipachika bao la pili
Wafungaji wakakutana live Nathan na Jerome
Wachezaji wa Boro hoi!!
Mashabiki nao wakazimika!!
Taswira Meneja wakiwajibika Uwanjani!
Jerome alipumzishwa!
0 maoni:
Chapisha Maoni