Chupchupuu!!!Marouane
Fellaini aliifungia Manchester United bao la pili na kufanya 2-1 dakika
ya 78 na mtanange kumalizika United wakiibuka kidedea kwenye Uwanja wa
Selhurst Park, London mbele ya mashabiki 25009. Ushindi huu wa United
unawapa Matumaini ya Kucheza Klabu Bingwa Ulaya msimu Ujao kwani
wamefanikiwa kupata pointi 68 na wapo ndani nne bora wakiwa pia nafasi
ya nne. Ashley Young akishangilia!Jason Puncheon dakika ya 57 kipindi cha pili alisawazisha bao na kufanya 1-1.Jason Puncheon akishangilia bao lake1-1Jason Puncheon baada ya kuweka sare Juan Mata akichonga penati.Mpaka nyavuni!Mata akishangiliaPongezi kwa MataMchezo
huu pia Umemalizika ukimwachia Majeraha Luke Shaw na kulazimika
kuondolewa Uwanjani na huku Wayne Rooney akipumzishwa baada ya kuumia
Mguu.Luke Shaw kaumia tena na Hapa ni Dokta akimcheki kwa karibu sanaLuke Shaw kaumia tena na kulazimika kuondolewa UwanjaniMeneja wa Newcastle United Alan Pardew alipata muda akateta na wachezaji wake na kuwapa mbinuLuke Shaw akiondolewa Uwanjani huko Ugenini Selhurst ParkRooney nae yale yale!Rooney alipumzishwa! Wachezaji wa Crystal Palace wakimsimamia Mwamuzi Michael Olivier baada ya kutoa penati kwa UnitedJuan
Mata dakika ya 19 kipindi cha kwanza aliifungia United bao kwa mkwaju
wa penati nao Crystal Palace walisawazisha kupitia mpira wa adhabu frii
kiki iliyofungwa na Jason Puncheon dakika ya 57 kipindi cha pili na
kufanya 1-1.Van Gaal akisalimiana na Meneja mwenzie Alan Pardew
0 maoni:
Chapisha Maoni