By:
Unknown
On: Jumamosi, Februari 25, 2017
Dabi
ya Kariakoo uliochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Leo
ulishuhudia Mtu Simba ikitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuichapa Yanga 2-1.
Yanga
walifunga Bao lao Dakika ya 5 kwa Penati ya Simon Msuva iliyotolewa baa
Fowadi wao Obrey Chirwa kuangushwa na Beki Novatus Lufunga. Dakika
ya 55 Simba walibaki Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Janvier Besala
Bokungu kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya kulambwa Kadi za Njano
2.
Simba wakasawazisha Bao Dakika ya 66 kupitia Laudit Mavugo
aleingizwa Kipindi cha Pili na kufunga Bao la Pili na la ushindi Dakika
ya 81 Mfungaji akiwa Shiza Kichuya.
VPL, inayoshirikisha Timu 16,
sasa inaongozwa na Simba wenye Pointi 54 kwa Mechi 23 na Yanga ni wa
Pili wakiwa na Pointi 49 kwa Mechi 22 huku Azam FC ni wa 3 wakiwa na
Pointi 41 kwa Mechi 23. VIKOSI:
SIMBA:
Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty
Lufunga [Shiza Kichuya, 51’], Abdi Banda, James Kotei, Ibrahim Hajib,
Muzamil Yassin, Juma Luizio [Said Ndemla, 27’], Laudit Mavugo, Mohammed
‘Mo’ Ibrahim [Jonas Mkude, 57’].
YANGA: Deogratius
Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Haji, Andrew Vincent, Kevin Yondan,
Justine Zulu [Juma Mahadhi, 78’], Simoni Msuva, Thabani Kamusoko [Said
Juma ‘Makapu’, 45’], Amisi Tambwe [Deus Kaseke, 70’], Obrey Chirwa,
Haruna Niyonzima.
REFA: Mathew Akrama [Mwanza]
WASAIDIZI: Mohammed Mkono [Tanga] na Hassan Zani [Arusha]
By:
Unknown
On: Jumanne, Februari 21, 2017
Kocha wa Man United Jose Mourinho kuelekea mchezo wao wa marudiano wa Europa League dhidi ya St Etienne ya Ufaransa, ameulizwa maswali kuhusu hatma ya nahodha wa Man United Wayne Rooney kama ataondoka katika timu hiyo au atabaki.
Jose Mourinho ambaye inaaminika ndio anaweza akafanya Rooney
aondoke mwisho wa msimu kama inavyoripotiwa au akabaki, ameshindwa
kuweka wazi kama ataondoka staa huyo au atabaki, lakini amekiri kuwa
hawezi kumlazimisha mchezaji kuhama.
“Kuhusu kuondoka unaweza kumuuliza mwenyewe kwa sababu
hata mimi siwezi kukuhakikishia kama nitakuwa hapa wiki ijayo, sasa
nawezaje kukuhakikishia kuwa mchezaji ataendelea kuwepo msimu ujao, kama
Rooney ataamua kuondoka sio kwa sababu mimi nataka aondoke”
“Hicho ndio ninachoweza kukuhakikishia sitaweza
kulazimisha legend wa Club hii kwenda sehemu nyingine, hivyo unaweza
kumuuliza Rooney mwenyewe kama angependa kumaliza soka lake katika timu
hii? lakini mimi nina furaha kuwa nae katika timu”
By:
Unknown
On: Jumatatu, Februari 13, 2017
UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku
Mechi za Kwanza
Jumanne 14 Februari 2017
Benfica v Borussia Dortmund
Paris Saint Germain v Barcelona
Jumatano 15 Februari 2017
Bayern Munich v Arsenal
Real Madrid v Napoli
Raundi
ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, inaanza Jumanne Usiku
kwa Mechi mbili na Jumatano pia zipo Mechi mbili na kuendelea Wiki
ijayo, zote zikiwa ni Mechi za Kwanza za Raundi hiyo.
Jumanne ni
huko Portugal wakati Benfica wakiikaribisha BVB Borussia Dortmund na
nyingine ni huko Jijini Paris, Paris pale Paris Saint Germain wakicheza
na Barcelona.
Jumatano pia zipo Mechi 2 za Raundi hii ambapo huko
Germany ni Bayern Munich na Arsenal na nyingine ni kule Santiago
Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain kati ya Real Madrid na Napoli ya
Italy.
Mechi za Kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UCL zitakamilika Wiki ijayo, Jumanne na Jumatano kwa Mechi 4.
Dondoo Muhimu:
Benfica v Borussia Dortmund
Mechi hii itachezwa huko Estádio do Sport Lisboa e Benfica, Lisbon na kuchezeshwa na Refa mzoefu kutoka Italy Nicola Rizzoli.
Timu hizi zimekutana mara 2 Ulaya na kila moja kushinda mara moja.
Benfica
watatinga kwenye Mechi hii wakiwakosa Andrija Zivkovic, alie Kifungoni,
na Majeruhi Lisandro Lopez huku Jonas akiwa kwenye hatihati kucheza
kutokana na maumivu.
Nao BVB watawakosa Majeruhi Mario Götze na Sven Bender huku hatihati ikiwa kwenye maumivu Nuri Şahin na Sebastian Rode.
Paris Saint Germain v Barcelona
Mechi hii ipo ndani ya Parc des Princes Jijini Paris Nchini France na itachezeshwa na Refa Szymon Marciniak kutoka Poland.
Katika Mechi zilizopita, PSG ilishinda mara 2, Sare 3 na Barca kushinda 4 kati yao.
PSG
kwenye Mechi hii itamkosa Thiago Motta ambaye yupo Kifungoni wakati
Barca watawakosa Majeruhi Arda Turan, Javier Mascherano na Aleix Vidal. UEFA CHAMPIONS LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku
Mechi za Kwanza
Jumanne 21 Februari 2017
Bayer 04 Leverkusen v Atlético Madrid
Manchester City v Monaco
Jumatano 22 Februari 2017
FC Porto v Juventus
Sevilla v Leicester City
Mechi za Pili
Jumanne 7 Machi 2017
Arsenal v Bayern Munich
Napoli v Real Madrid
Jumatano 8 Machi 2017
Barcelona v Paris Saint Germain
Borussia Dortmund v Benfica
Jumanne 14 Machi 2017
Juventus v FC Porto
Leicester City v Sevilla
Jumatano 15 Machi 2017
Atlético Madrid v Bayer 04 Leverkusen
Monaco v Manchester City
By:
Unknown
On: Jumatatu, Februari 13, 2017
Antonio
Conte amesema hapendi 'mzaha'wa Jose Mourinho baada ya Meneja huyo wa
Manchester United kudai Chelsea ambao ni Vinara wa EPL, Ligi Kuu
England, hawawezi kukamatika kileleni kwa sababu ni Timu 'inayojihami
mno!'.
Hivi sasa Chelsea wapo Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham baada Jana kutoka 1-1 na Burnley huko Turf Moor.
Mourinho,
ambae anasifika kwa kuchota akili za Mameneja wapinzani na kuwavuruga,
Juzi alidai Chelsea haiwezi kuteleza kutoka kileleni kwa vile
'wanajihami mno' na kushinda kwa kutumia 'kaunta ataki'.
Jana Meneja wa Chelsea Antonio Conte alijibu mapigo kwa kusema: "Hiyo ni hadaa yake. Nina uzoefu kuelewa hilo!"
Mara
nyingi Mourinho amekuwa akikwaruzana na Mameneja wenzake kutokana na
vijembe vyake vya kuwapandisha munkari ili kushinda vita ya kisaikolojia
na muhanga mkuu wa mashambulizi hayo huko nyuma akiwa Arsene Wenger wa
Arsenal. Hata hivyo Conte amegoma kuburutwa kwenye vita hiyo na kujibu: "Sipendi kujibu kuhusu Makocha wengine!"
EPL – Ligi Kuu England
RATIBA:
Jumatatu Februari 13
2300 Bournemouth v Manchester City
Jumamosi Februari 25
1800 Chelsea v Swansea City
1800 Crystal Palace v Middlesbrough
1800 Everton v Sunderland
1800 Hull City v Burnley
Southampton v Arsenal [IMEAHIRISHWA]
1800 West Bromwich Albion v Bournemouth
2030 Watford v West Ham United
Jumapili Februari 26
1630 Tottenham Hotspur v Stoke City
Manchester City v Manchester United[IMEAHIRISHWA]
Jumatatu Februari 27
2300 Leicester City v Liverpool
Jumamosi Machi 4
1530 Manchester United v Bournemouth
1800 Leicester City v Hull City
1800 Stoke City v Middlesbrough
1800 Swansea City v Burnley
1800 Watford v Southampton
1800 West Bromwich Albion v Crystal Palace
2030 Liverpool v Arsenal
Jumapili Machi 5
1630 Tottenham Hotspur v Everton
1900 Sunderland v Manchester City
Jumatatu Machi 6
2300 West Ham United v Chelsea
By:
Unknown
On: Jumatatu, Februari 13, 2017
Chelsea Leo wameikosa nafasi ya kwenda Pointi 12 mbele baada ya kutoka Sare na Burnley huko Turf Moor.
Chelsea
sasa wako Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham lakini Jumatatu
Usiku Manchester City wanaweza kutwaa Nafasi ya Pili na pengo lao na
Chelsea kuwa Pointi 8 ikiwa wataifunga Bournemouth Ugenini.
Hii
Leo Chelsea walitangulia kufunga Dakika ya 7 kwa Bao la Pedro lakini
Robbie Brady akaisawazishia Burnley Dakika ya 24 kwa Frikiki kali.
Matokeo haya yanawaweka Burnley Nafasi ya 12 na kudumisha rekodi yao ya kuwa wagumu mno wakiwa kwao Turf Moor.
By:
Unknown
On: Jumapili, Februari 05, 2017
By:
Unknown
On: Jumapili, Februari 05, 2017
Ibra akishangilia bao lake MANCHESTER
UNITED imewatandika Mabingwa wa England Leicester City 3-0 wakiwa kwao
King Power Stadium kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
Ushindi
huu umewabakiza Man United Nafasi ya 6 lakini sasa wapo Pointi 1 nyuma
ya Timu ya 5 Liverpool, Pointi 2 nyuma ya Timu ya 4 Arsenal, Pointi 4
nyuma ya Timu ya 3 Man City na Pointi 5 nyuma ya Timu ya Pili Spurs huku
Chelsea wakiwa kileleni Pointi 14 mbele ya Man United.
Man
United walipata Bao lao la kwanza Dakika ya 41 baada ya Kichwa cha Chris
Smalling kuwahiwa na Mkhitaryan kabla Beki wa Leicester Huth kuukuta
Mpira na kumtoka Beki mwingine wa Leicester Morgan na kumchambua Kipa
Schmeichel.
Sekunde 87 baada ya Bao hilo Man United walikuwa 2-0 mbele kwa Bao la Zlatan Ibrahimovic alieunganisha Krosi ya Valencia.
Hadi Mapumziko Leicester 0 Man United 2.
Kipindi
cha Pili kuanza Timu zote zilifanya mabadiliko kwa Leicester kuwaingiza
King na Gray kuwabadili Musa na Okazakina huku Man United wakimtoa
Marcos Rojo na kumwingiza Daley Blind.
Man United walifunga Bao la 3
Dakika ya 49 kufuatia ushirikiano mwema wa Ibrahimovic na Mkhitaryan
kumfungulia Juan Mata kupiga Bao.
By:
Unknown
On: Jumapili, Februari 05, 2017
By:
Unknown
On: Ijumaa, Februari 03, 2017
By:
Unknown
On: Ijumaa, Februari 03, 2017
EGYPT
wametinga Fainali ya AFCON 2017, Kombe la Mataifa ya Afrika, nah ii ni
mara yao ya 9 kufanya hilo na kuikuta Rekodi ya kucheza Fainali nyingi
baada ya Jana huko
Stade de I'Amitie, Libreville Nchini Gabon
kuibwaga Burkina Faso 4-3 kwa Mikwaju ya Penati Tano Tano kufuatia Sare
ya 1-1 katika Dakika 120.
Kipa Vterani wa Egypt, Essam El Hadary,
mwenye Miaka 44, ndie alikuwa Shujaa kwa kuokoa Penati ya Bertrand
Traore na kuwapa Egypt ushindi. Katika
Mechi hiyo, Egypt walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 65 la
Mohamed Salah na Burkina Faso kusawazisha Dakika ya 72 kupitia Aristide
Bance.
Kwenye Fainali, Egypt watapambana na Mshindi kati ya Ghana na Cameroon wanaopambana Leo huko Libreville, Gabon. VIKOSI:
BURKINA FASO:Koffi,
Yago, Dayo, B. Koné, Y. Coulibaly, Kaboré, I. Touré, R. Traoré (Diawara
80'), B. Traoré, Bancé (A.Traore 102'), Nakoulma.
EGYPT:El-Hadary,
El Mohamady (Gaber 106'), Hegazy, Gabr, Fathy, Hamed, M. Salah, I.
Salah, Said, Trezeguet (Sobhi 85'), Kahraba (Warda 76')
AFCON 2017
RATIBA
Robo Fainali
Jumamosi Januari 28
Burkina Faso 2 Tunisia 0 [RF 1]
Senegal 0 Cameroon 0 [Penati 4-5] [RF 2]
Jumapili Januari 29
Congo DR 1 Ghana 2 [RF 3]
Egypt 1 Morocco 0 [RF 4]
Nusu Fainali
Jumatano Februari 1
Burkina Faso 1 Egypt 1
Alhamisi Februari 2
2200 Cameroon v Ghana
Mshindi wa 3
Jumamosi Februari 4
2200 Burkina Faso v Aliefungwa NF 2
Fainali
Jumapili Februari 5
2200 Egypt v Mshindi NF 2
NCHI ZILIZOWAHI KUTWAA UBINGWA WA AFRIKA:
-Egypt-Mara 7
-Cameroon, Ghana-Mara 4
-Nigeria-Mara 3
-Congo DR-Mara 2
-Zambia, Algeria, Congo, Ethiopia, Ivory Coast, Morocco, South Africa, Sudan, Tunisia-Mara 1
By:
Unknown
On: Ijumaa, Februari 03, 2017
By:
Unknown
On: Ijumaa, Februari 03, 2017
Ligi
Kuu England imeendelea Jana kwa Mechi 3 na Manchester City kuibuka
washindi wakubwa kwa kuicharaza West Ham 4-0 wakati Manchester United
ikitoka 0-0 na Hull City na Stoke City na Everton kutoka 1-1.
Huko
London Stadium Jijini London, Wenyeji West Ham walibandikwa Bao 4-0 na
Man City kwa Bao za Kevin De Bruyne, David Silva, Gabriel Jesus na Yaya
Toure.
Matokeo hayo yamewabakisha City Nafasi ya 5.
Huko Old
Trafford, Kipa wa Hull City Eldin Jakupovic aliikosesha ushindi Man
United kwa kuokoa Bao za wazi kadhaa na hasa michomo ya Zlatan
Ibrahimovic na Paul Pogba. Matokeo
hayo yamewabakisha Man United Nafasi ya 5 ingawa hawajafungwa katika
Mechi zao 14 zilizopita za Ligi lakini Sare hii ya 3 mfululizo ndio
inawatafuna na kuwabakisha Nafasi hiyo ya 6 wakiwa Pointi 4 nyuma ya
Timu ya 5 City na Liverpool zinazofungana kwa Pointi.
Huko
Britannia Stadium, Wenyeji Stoke City na Everton zilitoka Sare 1-1 na
Wafungaji walikuwa Peter Crouch kwa Stoke na Ryan Shawcross aliejifunga
mwenyewe kuisawazishia Everton.
Kwa Crouch, hilo lilikuwa Bao lake la 100 la Ligi.
EPL – Ligi Kuu England
RATIBA
Jumamosi Februari 4
1530 Chelsea v Arsenal
1800 Crystal Palace v Sunderland
1800 Everton v Bournemouth
1800 Hull City v Liverpool
1800 Southampton v West Ham United
1800 Watford v Burnley
1800 West Bromwich Albion v Stoke City
2030 Tottenham Hotspur v Middlesbrough
Jumapili Februari 5
1630 Manchester City v Swansea City
1900 Leicester City v Manchester United
By:
Unknown
On: Ijumaa, Februari 03, 2017
Emmanuel Adebayor amejiunga na Timu ya Istanbul Basaksehir