.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Ijumaa, 29 Mei 2015

Tagged Under:

FA CUP-FAINALI JUMAMOSI-ARSENAL vs ATON VILLA, NANI KUIBUKA KIDEDEA!

By: Unknown On: Ijumaa, Mei 29, 2015
  • Share The Gag

  • Jumamosi Mei 30, Uwanjani Wembley, Jijini London kuanzia Saa 1 na Nusu Usiku, Arsenal na Aston Villa zitagombea FA CUP kwenye Fainali na tayari vijembe vishaanza kutembea.
    Mchezaji wa Aston Villa, Ashley Westwood, ameonya kuwa Wachezaji wa Arsenal hivi sasa hawapati usingizi kwa kumwota Straika hatari wa Villa Christian Benteke.

    Benteke ni Straika wa Ubelgiji mwenye Miaka 24 na ameshapiga Bao 12 katika Mechi zake 12 zilizopita baada ya kupona maumivu yake.
    Westwood amesema: "Benteke sasa amerejea katika ubora wake. Arsenal hawatapenda kucheza nae."
    Mwanzoni mwa Msimu, chini ya Meneja alietimuliwa Paul Lambert, Benteke alififia na kisha kuandamwa na Majeruhi lakini sasa chini ya Meneja mpya, Tim Sherwood, Straika huyo ameibuka upya.

    Lakini Westwood ameonya pia kuwa Timu yao si Benteke peke yake kwani wanao Fabian Delph, Tom Cleverly, Mchezaji wa Mkopo kutoka Man United, na Chipukizi Jack Grealish mwenye Miaka 19 ambae aling'ara mno kwenye Nusu Fainali ya FA CUP Villa ilipoibwaga LIverpool 2-1.Christian Benteke

    0 maoni:

    Chapisha Maoni