.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumamosi, 30 Mei 2015

Tagged Under:

KUWAACHA WACHEZAJI WALIOMALIZA MIKATABA YAO NA WENGINE KUENDELEA KUBAKI.

By: Unknown On: Jumamosi, Mei 30, 2015
  • Share The Gag
  • KAMATI YA UTENDAJI YA COASTAL UNION KUHUSU

    download (3) 
    NA MWANDISHI WETU,TANGA.
    Kikao cha Kamati ya Utendaji cha Coastal Union ambacho kimeketi
    katikati ya wiki hii chini ya Makamu Mwenyekiti wa Coastal Union,
    Steven Mguto kimeazimia kuwaacha baadhi ya wachezaji ambao muda wao
    ulikuwa umemalizika huku wengine wakiongezewa mikataba ya kuendelea
    kuitumikia timu hiyo kwa msimu ujao.
    Kimsingi wachezaji hao wameachwa na sasa wapo huru kutumikia timu
    nyengine ambazo zitahitaji huduma zao
    Akizungumza na waandishi wa habari leo, Ofisa Habari wa Coastal
    Union,Oscar Assenga amesema
    kuwa maamuzi hayo yalifikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya
    klabu hiyo ambacho kilifanyika juzi mkoani hapa.
    Amesema kuwa kimsingi katika kikao hicho kiliridhia kuwaacha wachezaji
    waliomaliza mikataba yao ikiwemo Shabani Kado,Keneth Masumbuko,Yayo
    Kato Lutimba, Seleimani Kibuta,Bakari,Razack Khalfani,Itubu Imbem na
    Othumani Tamimu.
    Aidha amesema kuwa wachezaji wengine ambao klabu imeamua kuwaacha ni
    Hussein Sued, Mansour Alawi, Amani Juma, Mohamedi Mtindi na Mohamed
    Hassani.
    Hata hivyo amesema wachezaji ambao wamemaliza mikataba yao ambao klabu
    ipo kwenye mazungumzo nao kwa ajili ya msimu ujao ni Bakari Mtama,Rama
    Salim, Godfrey Wambura na Joseph Mahundi.
    Wakati huo huo, uongozi wa Coastal Union umewapandisha timu wachezaji
    wanne kutoka timu ya vijana kucheza timu ya wakubwa ambao ni Mtenje
    Albano, Tumaini Karim, Mohamed Twaha Shekue “Djong”, Fikirini
    Suleiman“Mapara”

    0 maoni:

    Chapisha Maoni