.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 31 Mei 2015

Tagged Under:

KOMBE LA FA CUP LABATIZWA 'EMIRATES FA CUP'

By: Unknown On: Jumapili, Mei 31, 2015
  • Share The Gag

  • Kombe kongwe Duniani, FA CUP, kuanzia Msimu ujao litaitwa EMIRATES FA CUP.
    Kombe hilo, ambalo lilianza Mwaka 1871-1872, limekuwa halina Mdhamini tangu Msimu uliopita baada ya Kampuni ya Bia, Budweiser, kumaliza Mkataba na FA, Chama cha Soka England.
    FA sasa imeingia Mkataba na Kampuni ya Ndege ya Dubai, Emirates, kuwa Wadhamini wa Kombe hilo kwa Miaka Mitatu hadi 2018.
    Habari hizi za udhamini huu zimethibitishwa na Mwenyekiti wa FA, Greg Dyke, ambae amesema Kampuni ya Ndege ya Emirates ina nia njema kwenye Michezo na ni habari njema kwao, Washabiki na Gemu nzima ya Soka.

    Nae Rais wa Emirates, Sir Tim Clark, amesema Soka lina mvuto Dunia nzima na huunganisha jumuia nyingi na Nchi nyingi Duniani na hilo limethibitishwa na kuwa na Watazamaji zaidi ya Watu Bilioni 1.1.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni