
.jpg)
Nooij raia wa Uholanzi ambaye kikosi chake hakikufanya vizuri katika michuano ya kusaka taji la COSAFA baina ya mataifa ya Kusini mwa Afrika na kuondoka bila ya kupata ushindi wowote.
Michuano ya CHAN huwahusisha wachezaji wanaocheza soka katika vlabu vya nyumbani barani Afrika, na michuano ya mwaka 2016 itachezwa nchini Rwanda kuanzia mwezi Januari.
Mwaka 2009 wakati michuano hii ilipofanyika nchini Sudan, Tanzania ilifuzu katika michuano hiyo baada ya kuifunga Uganda mabao 3 kwa 2 lakini mwaka 2014, Uganda waliibuka washindi baada ya kuwachabanga Tanzania kwa jumla ya mabao 3 kwa 1 na kufuzu katika fainali hizo nchini Afrika Kusini.

0 maoni:
Chapisha Maoni