.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 16 Agosti 2015

Tagged Under:

SIMBA YATAKATA TAIFA LEO, YAIFUNGA URA 2-1

By: Unknown On: Jumapili, Agosti 16, 2015
  • Share The Gag

  • KLABU ya Simba imeendeleza wimbi la ushindi kwenye mechi za kirafiki baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya URA ya Uganda.
    Kwenye mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam mabao ya Simba yalifungwa na Kelvin Ndayisenga kwenye dakika ya nne ya mchezo huo na bao la pili likiwekwa kimiani na beki Juku Mushood kutoka Uganda.
    Bao la la URA lilifungwa na Kalanda Frank kwenye dakika ya 19 baada ya kutokea piga nikupige kwenye lango la Simba na mfungaji kupiga mpira uliompita kipa Peter Manyika na kuzaa bao hilo.
    Mchezo huo ulianza kwa kasi huku timu zote zikishambuliana kwa zamu ingawa waliwa Simba waliotangulia kufunga kwenye dakika ya nne na mchezaji wao mpya Kelvin Ndayisiyenga kuiandikia timu hiyo bao la kuongoza.
    Hata hivyo bao hilo lilidumu kwa dakika 15 kwani URA walifanikiwa kusawazisha kupitia kwa mshambuliaji wake Kalanda Frank baada ya kutokea piga nikupige kwenye lango la Simba.
    Baada ya bao hilo timu hizo zilishambuliana kwa zamu na dakika ya 36 Simon Sserunkuma anakosa bao la wazi lakini mpira alilopiga lilikwenda pembeni ya lango la URA kabla ya shuti dhaifu la Abdi Banda kudakwa na kipa wa URA Mwete Brian.

    Kalanda Frank alikaribia kuifungia URA bao la pili lakini shuti lake liligonga mwamba na kuokolewa na mabeki wa Simba na dakika ya 42 Kagimu Fatiq alipiga mpira ulioishia mikononi mwa kipa Peter Manyika.
    Kipindi cha pili kilianza kufanya mabadiliko saba kwa kuwapumzisha Awadh Juma na kuingia Said Ndemla, Abdi Banda akaingia Justice Majibva, Issa Abdallah akaingia Mwinyi Kazimoto, Emery Nimuboma akaingia Ramadhani Kessy, Samih Nuhu akaingia Mohamedi Hussein, Simon Sserunkuma akaingia Peter Mwalyanzi na Said Issa akaingia Hassan Isihaka.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni