Bao!!
Jonas Olsson dakika ya 64 aliipa bao West Brom Albion baada ya kutokea mpira wa Adhabu nje kidogo na box na kuachia shuti kali lililombabatiza mchezaji kwenye ukuta na kuzama moja kwa moja nyavuni mwa lango la Man United na kufanya 1-0.
Manchester
United walitawala kila kitu na pia kupata Penati, Manchester United
wamejikuta wakichapwa Bao 1-0 kwao Old Trafford na West Bromwich Albion
na kufungua matumaini makubwa kwa Liverpool na Tottenham kuweza
kuwaporomosha kutoka Nafasi ya 4 ya Ligi Kuu England.
Bao la ushindi la WBA lilifungwa Dakika ya 64 baada Frikiki ya Chris Brunt kumbabatiza Jonas Olsson na kutinga.
Man United walipata Penati Dakika ya 74 na Robin van Persie kupiga na Kipa Myhill kuokoa.
Matokeo
haya yamewaacha Man United, ambao sasa wameshushiwa kipigo chao cha 3
mfululizo, Nafasi ya 4 wakiwa Pointi 4 juu ya Liverpool huku wote
wakibakisha Mechi 3.
Wachezaji wa West Brom wakimtinga mwamuzi baada ya kutoa penati
Aaa!! Wachezaji wa West Brom wakipongezana
Taswira mpaka bao linapatikana kwenye ukuta baada ya kupigwa kwa mpira wa Adhabu
ikichongwa!
Robin Van Persie akiachia shuti kali
Meneja wa Man United Louis Van Gaal
Ander H. akifanya yake
Robin Van Persie na Rooney walianza katika mechi hii
Mapumziko, Manchester United 0 vs 0 West Brom
Wakiingia..
Mashabiki wa Man United
Mashabiki wa Man United wakiwa kimya!
VIKOSI:Manchester United wanaoanza: De Gea, Valencia, Smalling, McNair, Blind, Ander Herrera, Mata, Rooney, Fellaini, Young, Van Persie
MUFC akiba: Jones, Di Maria, Falcao, Januzaj, Valdes, Blackett, Pereira
West Brom wanaoanza: Myhill, Dawson, McAuley, Olsson, Lescott, Gardner, Yacob, Fletcher, Mulumbu, Brunt, Berahino
WBA akiba: Wisdom, Baird, Ideye, Anichebe, McManaman, Sessegnon, Rose
0 maoni:
Chapisha Maoni