

Mbali ya kuwania kuwa Klabu ya kwanza kulibeba Kombe mara 4, Sevilla pia wanawania kulitwaa ili kuweza kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao kwani, kwa mara ya kwanza, Bingwa wa EUROPA LIGI anaingizwa UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.
Hii ni nafasi pekee kwa Sevilla ambao hivi Juzi walimaliza La Liga wakiwa Nafasi ya 5 na hivyo kukosa kuingizwa UEFA CHAMPIONS LIGI.

Hii ni mara ya kwanza kwa Dnipro kucheza Fainali ya Klabu Barani Ulaya.
Sevilla, chini ya Kocha Unai Emery, wamefika Fainali hii kwa kuzitoa Borussia Monchengladbach, Villarreal, Zenit St Petersburg na Nusu Fainali Fiorentina ambayo waliinyuka Jumla ya Mabao 5-0 na hiyo yote ni kutokana na kazi njema ya Wachezaji wao kina Carlos Bacca, Aleix Vidal, Kevin Gameiro na Jose Antonio Reyes.


0 maoni:
Chapisha Maoni