Kama ambavyo ilivyokuwa kwa upande wa bara la Afrika kuliwa na michezo kadhaa kupigwa weekend hii na bara la Ulaya ilipigwa michezo kadhaa ya kuwania kufuzu kucheza michuano ya Euro 2016. Timu ya taifa ya Uingereza Jumamosi ya Septemba 5 ilicheza mechi dhidi ya San Marino.
Nahodha wa Manchester United Wayne Rooney aliingia katika headlines baada ya kuifikia rekodi ya mfungaji bora wa muda wote katika timu ya taifa ya Uingereza Sir Bobby Charlton, rekodi ambayo inatajwa kudumu kwa muda wa miaka 45. Rooney aliifikia rekodi hiyo baada ya kufunga goli moja katika ushindi wa goli 6-0 dhidi ya San Marino.
0 maoni:
Chapisha Maoni