.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 20 Septemba 2015

Tagged Under:

CHELSEA 2 vs 0 ARSENAL

By: Unknown On: Jumapili, Septemba 20, 2015
  • Share The Gag

  • Chelsea Leo wameanza kufufua matumaini ya kutetea Taji lao baada ya kuwafunga Mahasimu wao wa Jijini London Mtu 9 Arsenal Bao 2-0 katika Mechi ya Ligi Kuu England iliyochezwa Uwanjani Stamford Bridge.
    Baada ya kuanza Hovyo kwa kufungwa Mechi 3, Sare 1 na Kushinda 1 tu na kujikuta wako Nafasi ya 17 wakiwa Pointi 11 nyuma ya Vinara Man City, Leo Chelsea walikamia ushindi na Diego Costa alihakikisha hilo baada ya kuwachokoza Mabeki wa Arsenal na kusababisha Sentahafu wao apande jazba na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.

    Katika Dakika ya 44 ilizuka purukushani kati ya Diego Costa wa Chelsea na Laurent Koscielny wa Arsenal na Costa kuonekana kumpiga Koscielny kisha kumusukuma kwa Kifua hadi chini lakini, kwa mshangao mkubwa, Refa Mike Dean hakumwadhibu Costa kama ilivyotegemewa na badala yake kuwapa Kadi za Njano Costa na Sentahafu wa Arsenal anaetoka Brazil Gabriel. Dakika moja baadae Gabriel alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya kumrushia teke Costa.
    Hadi Haftaimu, Chelsea 0 Arsenal 0.
    Kipindi cha Pili Dakika ya 53, Frikiki ya Fabregas iliunganishwa kwa Kichwa na Kurt Zouma na kuwapa Chelsea Bao.
    Dakika ya 79, Arsenal walibaki Mtu 9 baada ya Kiungo wao Santi Cazorla kupewa Kadi ya Njano ya Pili na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.

    Eden Hazard aliipa Chelsea Bao lao la pili katika Dakika ya 91 baada ya Shuti lake kumbabatiza Alex Oxlade-Chamberlain na kutinga.Eden HazardKurt Zouma aipatia bao la kuongoza Chelsea kipindi cha pili dakika ya 53, Bao la kichwa.Gabriel nje kwa kadi nyekundu!

    0 maoni:

    Chapisha Maoni