.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 20 Septemba 2015

Tagged Under:

MANCHESTER CITY 1 vs 2 WEST HAM UNITED, CITY WAPOTEZA KWA MARA YA KWANZA MSIMU HUU 2015/2016

By: Unknown On: Jumapili, Septemba 20, 2015
  • Share The Gag


  • Timu ya West Ham United sasa wamekuwa mafundi wa kuzibomoa Timu kubwa Nyumbani kwao Msimu huu baada ya Jana kuwatandika Vinara wa Ligi Kuu England Manchester City Bao 2-1 wakiwa kwao Etihad na kuwaonjesha kipigo chao cha kwanza kwenye Ligi Msimu huu.
    Kipigo hiki pia ni cha pili mfululizo kwa City ambao Kati-Wiki walichapwa 2-1 na Juventus hapo hapo Etihad kati Mechi ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONS LIGI.
    Katika Mechi yao ya kwanza Msimu huu, West Ham, wakicheza Ugenini huko Emirates, waliifunga Arsenal 2-0 na kisha huko Anfield kuibamiza Liverpool 3-0.
    Jana huko Etihad, West Ham, chini ya Meneja wao mpya kutoka Croatia Slaven Bilic, walitangulia kwa Bao 2 zilizofungwa na Mchezaji wa Mkopo kutoka Chelsea Victor Moses katika Dakika ya 6 na Diafra Sakho katika Dakika ya 31.
    Bao la City lilifungwa na Mchezaji wao mpya Kevin De Bruyne katika Dakika ya 46.
    Hadi Mapumziko City 1 West Ham 2.
    Kipindi cha Pili, City, waliocheza bila ya Mastaa wao Majeruhi, Vincent Kompany na David Silva, walikuja juu lakini West Ham walisimama kidete kulinda Bao zao.

    BAO la Victor MosesKocha wa West Ham United

    0 maoni:

    Chapisha Maoni