.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumatatu, 21 Septemba 2015

Tagged Under:

HUYU NDIYE JOGO FEIO, ARSENAL MBONA MNALIALIA….

By: Unknown On: Jumatatu, Septemba 21, 2015
  • Share The Gag

  • bazira.com
    CHELSEA iliyokuwa inayumba katika Ligi Kuu England ambayo wao ni mabingwa watetezi, imeibuka na kuitwanga Arsenal kwa mabao 2-0.


    Ushindi wa Chelsea huenda haukupewa nafasi kubwa kutokana na timu hiyo kuanza ligi kwa kusuasua, huku kocha wake, Jose Mourinho akionekana kutojielewa.

    Lakini sasa imeibuka na kushinda dhidi ya Arsenal iliyoonekana kubadilika na angalau kuanza kushinda dhidi ya Chelsea baada ya ushindi wake wa bao 1-0 dhidi ya vigogo hao wa Stamford Bridge kwenye mechi ya Ngao ya Jamii.

    Ajabu, wakati Chelsea inaibuka na ushindi, juzi, haujawa gumzo, badala yake kila mmoja anazungumzia kuhusiana na mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa.

    Kwamba raia huyo wa Hispania mwenye asili ya Brazil, alikuwa tatizo na alipaswa kupewa kadi nyekundu. Gumzo kwamba alisababisha beki Gabriel alambwe kadi nyekundu kwa kuwa aliparura shingoni, alimsukuma, pia alifanya ubabe kwa beki mwingine wa Arsenal, Laurent Koscielny.


    Katika purukushani hizo, Costa aliambulia kadi ya njano lakini Kocha Arsene Wenger amesema mshambuliaji huyo alistahili kadi nyekundu kabisa, huku akiamini mwamuzi Mike Dean na wasaidizi wake hawakuwa makini sana ingawa alikataa zaidi kuzungumzia kuhusu waamuzi.

    Kinachoweza kushangaza zaidi ni kwamba pamoja na kelele zote, Costa hakupatikana na faulo hata moja ukiachana na ile kadi. Hakuonekana kucheza madhambi au vinginevyo ingawa kweli purukushani zake ziliwavuruga kabisa Arsenal, wakashindwa kufikia malengo yao kiuchezaji.

    Nani kasahau ‘footbal is a game of contact’. Mtacheza vipi soka bila ya kugusana, angalau kusukumana au kuangushana? Mourinho alitolea mfano wa mchezo wa ‘badminton’, kwamba watu hawagusani na soka haiko hivyo. Sawa na hapa ungeweza kutolewa mfano wa draft!

    Utajiuliza hivi; hawa Arsenal walikuwa wanakutana kwa mara ya kwanza na Costa? Jibu, hapana, sasa vipi iwe ndiyo ishu wakati kuna kadi nyekundu nyingine ya Santi Cazorla ambayo iliwavuruga kabisa.



    Arsenal ni timu yenye mashabiki walalamishi kuliko wote duniani. Kama siyo, sasa vipi wanalialia, kwani hawakujipanga? Au waliingia uwanjani wakiwa hawajui wamejipangaje kukabiliana na jogo feio?

    Jina jogo feio kwa Lugha ya Kireno ni mchezaji mwenye mchezo wa vurugu, huo ni uchezaji wa Costa akiwa Hispania, jina ambalo linatambulika sana.

    Kuna ‘game plan’, yaani mipango ya mchezo. Arsenal lazima walijua Costa ndiyo atakuwa tatizo na atatumika kuwachanganya mabeki. Sasa vipi walikubali kuchanganywa kweli na kutoa nafasi Mhispania huyo auchukue mchezo wote?

    Costa ndiye aliyeipa Chelsea ushindi kwa kuwa ameonekana kuwa ‘profesheno’ zaidi ya wanavyomsema. Kwa sababu hizi tatu.


    Moja:
    Straika anatakiwa kuisaidia timu yake kupata ushindi kwa mambo matatu. Kufunga, kutoa pasi ya bao au kusaidia kuwavuruga mabeki wa timu pinzani.

    Yeye amefanikiwa kuwavuruga mabeki na kikosi kizima cha Arsenal, amepunguza mtu baada ya beki kutolewa.

    Mbili:
    Amewatoa Arsenal mchezoni, wamepaniki na kushindwa kucheza walivyotakiwa au kama walivyoanza kipindi cha kwanza:

    Tatu:
    Wenger pia alionekana kuingia kwenye mtego wa Costa. Badala ya kuendeleza mipango, akatumia muda mwingi kulalamika dhidi ya jogo feio akimuacha Mourinho akiendeleza mipango ya kummaliza.

    Sasa kwa Costa anataka nini zaidi? Kwa mashabiki na uongozi wa Chelsea anastahili pongezi kwa kazi nzuri.

    Ukiangalia hakumuumiza mtu, lakini amevuruga mbinu za wapinzani. Pia amekuwa akicheza hivyo na mifano utaona alipozozana nusura azichape na Steven Gerrard pale Chelsea walipokutana na Liverpool, msimu uliopita.

    Unakumbuka vita yake na beki Martin Skrtel wa Livepool au John O’shea wa Sunderland? Najua bado hujasahau vita yake na David Luiz wa PSG na vurugu nyingine kibao.

    Siku moja Costa hatakuwa shujaa, kwa kuwa anaweza akakosea hesabu na kusababisha alambwe kadi nyekundu kwa kuwa kwa kipindi hiki waamuzi watamtupia jicho kwa karibu kukwepa lawama anazosukumiwa Dean na wasaidizi wake.

    Ukweli ni kwamba sasa Costa ni shujaa wa Chelsea, hasa kwa mechi ya juzi na kama alivyosema Mourinho, kwamba alivyocheza Costa ilikuwa sahihi na ndiyo mipango hasa ya mchezo ilivyotakiwa iwe. Hivyo Arsenal, waache kulialia.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni