.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumatatu, 28 Septemba 2015

Tagged Under:

RATIBA UEFA CHAMPIONS LEAGE: KESHO

By: Unknown On: Jumatatu, Septemba 28, 2015
  • Share The Gag
  •   

    Jumanne zipo Mechi 8 za Makundi E hadi H na Jumatano ni 8 za Makundi hadi A hadi D.
    Mabingwa Watetezi Barca wako kwao Nou Camp kucheza na Bayer Leverkusen wakisaka ushindi wao wa kwanza baada ya kutoka Sare 1-1 na AS Roma katika Mechi yao ya kwanza ya kundi E Ugenini huko Italy.
    Lakini Barca watatinga Mechi hii bila ya tegemezi wao mkubwa Lionel messi ambae ameumia Goti na anakisiwa kuwa nje kwa kipindi cha hadi Wiki 8.
    Bayer Leverkusen walishinda Mechi yao ya kwanza kwa kuinyuka BATE Borislov 4-1.
    Kwenye Kundi F, Arsenal, baada ya kuchapwa 2-1 Dinamo Zagreb wako kwao Emirates kucheza na Olympiacos ambayo ilianza kwa kuchapwa kwao 3-0 na Bayern Munich ambao wanacheza Nyumbani huko Munich na Dinamo Zagreb.
    Chelsea, ambao walianza kwa kuinyuka Maccabi Tel Aviv 4-0 Uwanjani Stamford Bridge, wako Ugenini huko Ureno kucheza na FC Porto ambayo ndiyo Klabu iliyompa umaarufu Meneja wao wa sasa Jose Mourinho.
    FC Porto walianza kwa Sare ya 2-2 Ugenini na Dynamo Kiev. 


    UEFA CHAMPIONS LIGI
    RATIBA
    Jumanne 29 Septemba 2015

    KUNDI E
    Barcelona vs Bayer Leverkusen
    BATE Borislov vs AS Roma

    KUNDI F
    Arsenal vs Olympiakos
    Bayern Munich vs Dinamo Zagreb

    KUNDI G
    FC Porto vs Chelsea
    Maccabi Tel Aviv vs Dynamo Kiev

    KUNDI H

    Lyon vs Valencia
    Zenit St Petersburg vs KAA Gent

    Jumatano 30 Septemba 2015
    KUNDI A

    Malmö FF v Real Madrid
    Shakhtar Donetsk v Paris St Germaine

    KUNDI B
    CSKA v PSV
    Man United vs VfL Wolfsburg

    KUNDI C
    1900 FC Astana v Galatasaray
    Atletico Madrid vs Benfica

    KUNDI D
    Borussia Mönchengladbach vs Man City
    Juventus vs Sevilla

    0 maoni:

    Chapisha Maoni