.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumatatu, 28 Septemba 2015

Tagged Under:

MASHABIKI WATAKA PELLEGRINI ANG’OKE! NI BAADA YA KUPITWA KILELENI NA MAN UNITED, KIPIGO CHA 4-1 MASHABIKI WACHACHAMAA ETIHAD!

By: Unknown On: Jumatatu, Septemba 28, 2015
  • Share The Gag
  • MASHABIKI wa Manchester City sasa wamekuwa mbogo na kuanza kumshambulia Meneja wao Manuel Pellegrini baada ya Jumamosi kunyukwa 4-1 na Tottenham kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.
    Wiki mbili zilizopita Man City walikuwa kileleni mwa Ligi Kuu England baada ya kushinda Mechi zao zote 6 za Ligi Kuu England lakini sasa wamechapwa Mechi mbili mfululizo na kupokonywa uongozi wa Ligi na Mahasimu wao wakubwa Man United.
    Kwa Mashabiki wengi wa Man City kuporomoka kwao ni kosa la Manuel Pellegrini na uamuzi wake wa kumpiga Benchi Kipa wao Joe Hart na kumchezesha walipochapwa 4 na Spurs haukupokelewa vyema.

    Baadhi ya Mashabiki hao wamediriki hata kudai Pellegrini ni Meneja wa kawaida tu na hastahili kuongoza Timu yao yenye Wachezaji wenye hadhi ya Kisupastaa.Harry Kane

    0 maoni:

    Chapisha Maoni