
Msimu uliopita wa ligi kuu, kila timu shiriki iliruhusiwa kusajili wachezaji wageni wasiozidi watano lakini azimio jipya, ambalo bado vilabu wamelikubali, litatoa fursa ya kusajili wachezaji 10 katika kile kinachoonekana kuleta ushindani.
Mkurugenzi wa mashindano wa Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF), Boniface Wambura amesema azimio hilo litawasilishwa katika kamati ya utendaji kwa ajili ya kupata ridhaa.

Vilabu vikubwa nchini Tanzania kama vile Simba, Yanga na Azam zimekuwa zikisajili wachezaji wageni kwa ajili ya kuleta tija katika ushindani wao wa ndani na ule wa kimataifa.

0 maoni:
Chapisha Maoni