UONGOZI wa Coastal Union,Wagosi wa Kaya
umeingia mkataba wa miaka miwili na aliyekuwa Kocha Mkuu wa Kagera
Sugar, Jackson Mayanja kuifundisha timu ya Coastal Union katika msimu
ujao wa Ligi kuu soka Tanzania Bara itakayoanza Mwezi Agosti mwaka huu .
“Uwezo wa kocha Mayanja unatupa matumaini makubwa ya mafanikio ukizingatia ana uwezo wa kufundisha na kupata mafanikio hivyo tunaamini kuja kwake kwetu itakuwa chachu katika maendeleo”, alisema Assenga
Mayanja aliwahi kuzifundisha timu za soka Kiyuvu FC ya Rwanda,timu ya Mamlaka ya Mapato (URA),Vipers FC ya Bunamwaya na KCC zote za Uganda amesema kutua kwake kwenye timu Coastal Union kunampa faraja hivyo atahakikisha anatoa mchango wake kuipa mafanikio.
Pia alisema mipango yake ni kuhakikisha timu inang’ara katika michuano ya ligi kuu msimu ujao ikiwa ni pamoja na kubadili aina ya mchezo wa timu hiyo ili iweze kupata mafanikio kwa kuhirikiana na wachezaji, mashabiki na uongozi kwenye medani za kitaifa na kimataifa.
0 maoni:
Chapisha Maoni