.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Ijumaa, 19 Juni 2015

Tagged Under:

TIMU YA TAIFA YA UGANDA KUINUSURU TAIFA STARS NA KOCHA MKUU WAKE MART NOOIJ UWANJA WA AMANI VISIWANI ZANZIBAR ?.

By: Unknown On: Ijumaa, Juni 19, 2015
  • Share The Gag

  • Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, kesho inatarajiwa kushuka dimbani kucheza na timu ya Taifa ya Uganda katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainaili za wachezaji wa ndani CHAN 2016.


    Kikosi cha Taifa Stars kimeendelea na mazoezi katika uwanja wa Amani kisiwani Zanzibar kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa kuanzia majira a saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.


    Stars inahitaji ushindi katika mchezo huo wa awali ili kujiweka katika mzingira mazuri ya kusonga mbele, kabla ya mchezo wa marudaino utakaofanyika baada ya wiki mbili jijini Kampala.


    Kocha mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij amesema vijana wake wako katika hali nzuri kuelekea kwenye mchezo wa kesho, na kuwaomba watanzania kuwapa sapoti katika mchezo huo.


    Endapo Stars itaitoa Uganda katika hatua ya awali, itafuzu katika hatua ya pili ambapo itacheza dhidi ya timu ya Taifa ya Sudan, na mshindi wa mchezo huo moja kwa moja atafuzu kwa fainali za CHAN 2016 nchini Rwanda.

    Wakati huo huo, timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) inatarajiwa kuwasili leo mchana jijini Dar es salaam kisha kuelekea kisiwani Zanzibar tayari kwa mchezo huo wa kesho dhidi ya Taifa Stars.


    TWFA KUFANYA UCHAGUZI AGOSTI 15
    Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA), George Mushumba ametangaza uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika agosti 15, 2015 kujaza nafasi mbalimbali.


    Kwa mamlaka aliyonayo anapenda kutangaza uchaguzi mkuu wa TWFA leo kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi, uchaguzi huo utafanyika tarehe 15, Agosti 2015 katika nafasi zifuatazo:

    0 maoni:

    Chapisha Maoni