.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Ijumaa, 26 Juni 2015

Tagged Under:

UHAMISHO: MAN UNITED YAWAWEKA SAWA KIBEI REAL MADRID, SASA YATAKIWA WATOE PESA YA KUVUNJA REKORI YA £35M!

By: Unknown On: Ijumaa, Juni 26, 2015
  • Share The Gag

  • Manchester United imeionya Real Madrid kwamba wanapaswa kulipa zaidi ya ile Ada ya Uhamisho inayoshika Rekodi ya Dunia kwa Kipa ikiwa wanamtaka Kipa wao David De Gea.
    Habari zimedai ili kumng'oa Kipa huyo kutoka Spain huko Man United lazima Wanunuzi wavunje Rekodi ya ununuzi wa Kipa wa Italy Gianluigi Buffon iliyowekwa 2001 kwa kulipwa Pauni Milioni 32.6 aliponunuliwa kutoka Parma na kuhamia Juventus.
    Man United ilimnunua De Gea, mwenye Miaka 24, Mwaka 2011 kutoka Atletico Madrid kwa Dau la Pauni Milioni 18.9 na kumfanya awe Kipa wa Pili kwa Bei ghali Duniani nyuma ya Gianluigi Buffon.

    Inadaiwa msimamo wa Man United hivi sasa ni kutaka De Gea abaki na kumaliza Mkataba wake uliobakiza Miezi 12 na kisha kumpoteza bila kulipwa Fedha yeyote kuliko kumuuza sasa kwa Bei ya kutupwa.
    Hata hivyo, zipo kila dalili kuwa Kipa huyo atang'oka Old Trafford kwani hata Nyumba ya kupanga aliyokuwa akiishi huko Cheshire, Kitongoji jirani ya Jiji la Manchester, imetangazwa kuuzwa.
    De Gea ndie alietwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Man United kwa Misimu Miwili iliyopita na kukibeba sana Kikosi cha Meneja Louis van Gaal kufuzu 4 bora Msimu uliopita na kurudi tena kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao unaoanza Agosti.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni