.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumatano, 17 Juni 2015

Tagged Under:

Yanga kuivaa SC Villa Juni 27 2015

By: Unknown On: Jumatano, Juni 17, 2015
  • Share The Gag
  • index 

    ………………………………..
    MABINGWA wa soka wa Tanzania Bara, Yanga, Juni 27, mwaka huu wanatarajia kuvaana na SC Villa ya Uganda katika mchezo wa kirafiki utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ukiwa na lengo la kukusanya fedha za kujengea kituo cha watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na walemavu wa ngozi, yaani albino.
    Akizungumza Dar es Salaam jana katika ukumbi wa makao makuu ya Yanga yaliyopo Jangwani, jijini, Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Jonas Tiboroha, alisema kuwa katika mchezo huo watachezesha kikosi chao kamili, kikiwajumuisha wachezaji wapya na nyota wa zamani.
    Alisema wameamua kushiriki katika tamasha hilo kama sehemu ya kuonyesha jinsi wanavyoguswa na jamii, ikiwa ni baada ya kuombwa kufanya hivyo na Taasisi ya Nyumbani Kwanza Media kwani hata klabu kubwa Ulaya zimekuwa zikiafnya hivyo.
    “Baada ya kuletewa wazo hili na wenzetu wa Nyumbani Kwanza, tulikubaliana nao kwani ni zuri. Tumeona klabu ya Yanga isipate isipate sifa kwa kutwaa ubingwa tu, bali pia hata kufanya shughuli za kijamii kama hizi. Uongozi umebariki na hata Kocha Mkuu na benchi lote la ufundi lina taarifa na ndio maana tumeanza mazoezi mapema zaidi,” alisema.
    Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Nyumbani Kwanza Media, Mossy Magere, alisema kuwa wazo la kuandaa tamasha hilo lilikuja baada ya kutafakari ni vipi wanaweza kusaidia makundi yenye mahitaji maalumu na wakaona ni vema kuishirikisha Yanga wakiwa kama mabingwa wa Tanzania Bara.
    “Mapato yatakayopatikana yatafanya shughuli kusudiwa kwa kuanza rasmi ujenzi wa kituo huko Bagamoyo, mkoani Pwani na tutakuwa tukifahamishana kila hatua ya mradi huo utakaogharimu Sh bilioni 1.5 ambao tumepania uwe mfano wa kuigwa na wengine,” alisema Mossy.
    Aliwapongeza Yanga kwanza kwa kutwaa ubingwa wa Bara, lakini pia kukubali kushirikiana nao katika kufanikisha tamasha hilo la aina yake.
    Awali mechi hiyo ilikuwa ichezwe kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, lakini kutokana na ushauri wa Tiboroha, waliamua iwe Dar es Salaam ili kupunguza gharama za maandalizi yake, hasa katika suala zima la usafiri kwa timu na mengineyo.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni