.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumanne, 16 Juni 2015

Tagged Under:

PAMOJA NA KUKOSA TUNZO YA KILI KI MIZENGWE CHRISTIAN BELA APAGAWISHA TABORA!

By: Unknown On: Jumanne, Juni 16, 2015
  • Share The Gag


  • Christian Bella akijimwaga jukwaani.
    Masaa machache baada ya kukosa kitatanishi tunzo ya wimbo bora wa mwaka katika Kili Music Awards Christian Bela (King of melodies) alipagawisha wapenzi wa muziki mjini Tabora alipoporomosha bonge la show akiwa na kundi zima la Malaika Band.
    Christian Bela alitarajiwa na wadau wa muziki nchini kuwa angebeba tunzo hiyo bila ushindani mkubwa kutokana na wimbo wake wa Nani kama mama ambao aliomshirikisha Ommy Dimpoz kutamba sana katika vituo vyote vya redio na Runinga hapa nchini, lakini kama kawaida ya tunzo hizo zinazosimamiwa na BASATA na kudhaminiwa na kampuni ya utengenezaji bia ya Tanzania TBL zimekuwa zikilalamikiwa kila mwaka huku waanadaaji wakioneka kuweka pamba mbichi masikioni.
    Tunzo hiyo ya wimbo bora wa mwaka ilienda kwa wimbo wa Mwana wa msanii Ali Kiba. Onesho hilo lilifanyika katika viwanja vya Bwalo la Polisi Tabora.

    Bella akifanya yake jukwaani.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni