Baada ya makada mbalimbali
kutangaza nia na hatimaye kuchukua fomu za kugombea urais, Rapper Kala
Jeremiah amefunguka na kuwataka wananchi wote kuchagua kiongozi sahihi
mwenye sifa za kuingoza nchi.
Akizungumza na millardayo.com amesema ‘Tumchague
mtu na tusishawishike na vyama, tumchague mtu ambaye tuna mwamini,
Tanzania imefika sehemu ambayo sio sehemu nzuri sana kwa maana ya kwamba
tumekuwa tunaahidiwa vitu vingi sana mwisho wa siku bado wananchi
wanalalamika lakini pia kumekuwa na mikataba mingi ambayo hata wananchi
hawaijui kwa hiyo mtu anaposaini mkataba tulikuwa tunaomba wananchi
waipitie kwanza tuangalie faida za kiongozi
Kwa
hiyo naomba vijana wenzangu tusishawishe kisiasa tuangalie mtu ambaye
ana uwezo wa kuamua jambo sio tu kwasababu tumesikia ameongea vizuri
hapana tuangalie pia nyuma alishawahi kufanya kazi ipi ambayo
alitekeleza kwenye jamii, naamini safari hii wananchi wamtachagua
kiongozi atakayekuwa na misimamo sahihi ya kuwajibisha watu moja kwa
moja bila kuangalia usoni.
0 maoni:
Chapisha Maoni