

KOCHA Mkuu wa Toto African ya Mwanza, Martin Grelics kutoka Ujerumani, ameamua kubwaga manyanga kuifundisha timu hiyo.
Martin alifikia uamuzi wake huo jana, muda mfupi baada ya Toto African kuchapwa mabao 5-0 na Azam katika mechi ya ligi kuu iliyochezwa kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar esSalaam.
Hakuna taarifa zaidi iliyotolewa kuhusu sababu za kocha huyo kubwaga manyanga,lakini wachambuzi wa masuala ya soka wameeleza kuwa, haridhishwi na usimamizi na uendeshaji wa timu hiyo.
0 maoni:
Chapisha Maoni