Kikosi cha timu ya Taifa ya 
Tanzania, (Taifa Stars) kinachodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro 
kimeendelea kujifua katika uwanja wa Benki ya Biashara ya Ethiopia eneo 
la CMC asubuhi na jioni katika uwanja wa Taifa wa Addis Ababa.
Stars ambayo imeweka kambi jijini 
Addis Ababa imekua ikijifua mara mbili kwa siku, kuhakikisha wachezaji 
wanakua vizuri kuelekea katika mchezo dhidi ya timu ya Taifa  Misri 
mwishoni mwa wiki hii jijini Alexandria.
Hali ya kambi kiujumla ni nzuri, 
wachezaji wote ni wazima, wakiwa wenye ari, na morali ya hali ya juu 
katika maandalizi ya mchezo huo wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON 
mwaka 2017.
Kocha mkuu wa Taifa Stars 
mholanzi, Mart Nooij amekuwa akiwafundisha vijana wake mbinu mbali mbali
 kuelekea kwenye mechi dhidi ya Misri,  kuanzia sehemu ya ulinzi, kiungo
 na ushambuliaji kuhakikisha wanakua fit katika mchezo unaowakabili.
Ikiwa ni siku ya nne tangu Taifa 
Stars kuanza mazoezi yake jijini Addis Ababa, kocha Nooij amesema 
anashukuru vijana wake wanamuelewa vizuri anachowaelekeza, sasa timu 
inacheza mpira wa kasi na pasi za haraka haraka, vijana wamechangamka na
 morali ni ya hali ya juu kambini kuelekea kwenye mchezo unaowakabili.
Hali ya nidhamu kambini ni ya hali
 ya juu, wachezaji waanatambua umuhimu wa mchezo huo, na kikubwa 
wameahidi kupambana kusaka matokeo mazuri katika mchezo dhidi ya Misri.
“Katika mpira hakuna 
kinachoshindikana, sie tumejiandaa vizuri, naamini tutakapofika Misri 
tutafanya vizuri na kuwapa furaha watanzania, kikubwa watuombee kwa 
mwenyezi mungu, tuwe wazima mpaka siku ya mchezo, naamini tutafanya 
vizuri” alisema Nadri.
Stars inatarajiwa kuelekea jijini 
Cairo siku ya ijumaa, kisha kuunganisha katika jiji la Alexandria tayari
 kwa mchezo dhidi ya Misri utakaochezwa katika uwanja wa Boeg El Arab 
siku ya jumapili Juni 14, 2015.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 







 
0 maoni:
Chapisha Maoni