
Kwa muda mrefu iliaminika kuwa Pedro atatua Old Trafford huku kukiripotiwa kuwa tayari ameshaafikiana maslahi yake binafsi lakini kusita kwa Man United kulipa kwa mkupuo mmoja Dau ambalo Barca walikuwa wakitaka kumetoa mwanya kwa Chelsea kutumbukia na kukubali kulipa Dau hilo lote na kumnasa Staa huyo.

Kitu hicho Barca waligomea na kutaka Fedha zote kwa mkupuo na hapo ndipo Chelsea wakawapiku Man United.
Inatarajiwa wakati wowote kuanzia sasa Pedro, mwenye Miaka 28, atapimwa Afya yake huko Stamford Bridge na kisha kusaini Mkataba.
0 maoni:
Chapisha Maoni