.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 30 Agosti 2015

Tagged Under:

FULL TIME: SWANSEA CITY 2 vs 1 MANCHESTER UNITED,

By: Unknown On: Jumapili, Agosti 30, 2015
  • Share The Gag

  • 2-1Ayew akikatiza baada ya kuifunga bao la kusawazishaGomis  dakika ya 65 aliwapachikia bao la pili na kufanya 2-1 dhidi ya Man United.
    Kama ilivyokuwa Msimu uliopita, Leo tena Swansea City wametoka nyuma kwa Bao 1 na kuifunga Manchester United Bao 2-1 na kuishushia kipigo chao cha kwanza kwenye Ligi Kuu England kwa Msimu huu mpya.
    Hadi Mapumziko, Mechi hii iliyochezwa huko Liberty Stadium, ilikuwa 0-0.
    Dakika 3 tu baada ya Kipindi cha Pili kuanza Juan Mata aliipa Man United Bao ikiwa ni zawadi kwa kuitawala Mechi hii yote.
    Hadi Daki ya 60 Man United walionekana ni washindi lakini Dakika 1 baadae Mchezaji wa Kimataifa wa Ghana, Andre Ayew, akaisawazishia Swansea na Dakika 5 baadae, Mtu wao hatari, Bafetimbi Gomis akawapa Bao la Pili na la ushindi.

    A. Ayew kipindi cha pili aliwasawazishia bao Swansea kwa kichwa dakika ya 61 na kufanya 1-1.

    Kipindi cha pili dakika ya 48 juan mata aliwapachikia bao la kuongoza Man United na kufanya 1-0 dhidi ya Swansea City. Shaw alipiga krosi iliyompata Rooney kwa kuugusa na hatimae Juan Mata kuunganisha moja kwa moja ndani ya nyavu za Swansea City.Cgupuchupu Swansea wapate bao hapa kipindicha kwanza! Kipindi cha kwanza kimemalizika hakuna aliyeliona lango la mwenzake, Ngoma ilimalizika 0-0 s Man United wala Swansea.
    Swansea City wanahitaji Ushindi tena leo hii dhidi ya Man United, Je wataweza?
    Depay akiendesha mpira.
    Ligi Kuu England sasa inasimama kupisha Mechi za Kimataifa na itarejea tena Septemba 12 na Man United wapo kwao Old Trafford kupambana na Mahasimu wao wa Jadi Liverpool ambao Jana wakiwa kwao Anfield walinyukwa 3-0 na West Ham.VIKOSI:
    Swansea wanaoanza 11:
    Fabianski, Naughton, Fernandez, Williams, Taylor, Cork, Shelvey, Sigurdsson, Ayew, Routledge, Gomis
    Akiba: Nordfeldt, Rangel, Bartley, Tabanou, Ki Sung-Yueng, Dyer, Eder
    Manchester United wanaoanza 11: Romero, Darmian, Smalling, Blind, Shaw, Schneiderlin, Schweinsteiger, Mata, Herrera, Memphis, Rooney
    Akiba: Johnstone, McNair, Valencia, Carrick, Young, Fellaini, Chicharito

    0 maoni:

    Chapisha Maoni