.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 16 Agosti 2015

Tagged Under:

MANCHESTER CITY 3 vs 0 CHELSEA,

By: Unknown On: Jumapili, Agosti 16, 2015
  • Share The Gag
  • Sergio Aguero akishangilia bao lake la kwanza dhidi ya Chelsea.
    Mbele ya Mashabiki 54,331 Uwanjani kwao Etihad, Manchester City Leo wamewabonda Mabingwa wa England Chelsea Bao 3-0 katika Mechi ya Ligi Kuu England.
    Wakati huu ni ushindi wa pili mfululizo kwa City wa 3-0 kila Mechi tangu Ligi ianze Wikiendi iliyopita, kwa Chelsea hii ni Mechi yao ya pili bila ushindi baada kuanza kwa Sare ya 2-2 huko kwao Stamford Bridge walipocheza na Swansea City.
    Hii Leo City walistahili ushindi dhidi ya Chelsea ambayo kwenye Benchi lake Leo alikosekana Daktari wao Mwanamama maarufu Eva Carneiro ambae amepigwa marufuku na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho baada kutofautiana. Ramires katiMatic na Silva wakibananBaada ya Man City kupiga hodi mara kadhaa huku wakisimamishwa na ushujaa wa Kipa wa Chelsea Asmir Begovic ambae alikuwa Golini kuchukuwa nafasi ya Kipa Nambari Wani Thibaut Courtois aliefungiwa Mechi 1 baada ya Kadi Nyekundu katika Mechi iliyopita waliyotoka 2-2 na Swansea City, Man City walifanikiwa kufunga katika Dakika ya 31.
    Kweupeee 1-0
    1-0Bao hilo lilitokana na pasi safi ya David Silva na kumkuta Sergio Aguero alieachia shuti la chini na kutinga.
    Kipindi cha Pili kilianza kwa Chelsea kufanya kitu cha ajabu kwa kumpiga Benchi Nahodha wao John Terry na kumuingiza Kurt Zouma nah ii ni mara ya kwanza kwa Jose Mourinho kuwahi kumpumzisha Nahodha wake kwa staili hiyo.
    Kepteni wa Man City, Vincent Kompany aliipa Timu yake Bao la Pili katika Dakika ya 79 kwa kichwa baada ya kuunganisha Kona ya David Silva. Akipata matibabu kutoka kwa daktari wa timu
    Diego CostaDiego Costa chini!Dakika ya 84, City wakawa 3-0 mbele kwa Bao la Fernandinho aliefunga kwa shuti kutoka nje tu ya boksi.
    Vincent Kompany dakika ya 79 na Fernandinho dakika ya 85Hatari tupu!! 1-0Sergio Agüero dakika ya 31aliipatia bao la kuongoza na mtanange kwenda mapumziko ukiwa 1-0 dhidi ya Chelsea.2-0 Kompany akiwachoma bao ChelseaVicent Kompany akishangilia bao lake la piliBao la pili kwa Kompany msimu huu mpya Ligi Kuu England3-0

    0 maoni:

    Chapisha Maoni