.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Alhamisi, 13 Agosti 2015

Tagged Under:

Huu ni ushauri wa Rais wa FIFA kwenda kwa nchi za Ulaya Magharibi…

By: Unknown On: Alhamisi, Agosti 13, 2015
  • Share The Gag
  • Kutoka makao makuu ya shirikisho la soka ulimwenguni FIFA, Rais wa FIFA Sepp Blatter ametoa ushauri kwa nia njema kwa nchi za Ulaya Magharibi kuiga na kujifunza kitu kutoka katika nchi ya Urusi ambayo sheria ya soka ya nchi hiyo ina ruhusu idadi maalumu ya wachezaji wa kigeni kucheza katika mechi moja.
    Kupitia katika Magazine ya FIFA Blatter alishauri kujali vipaji vya nchi husika kwa kuwapa nafasi ya kucheza zaidi kiasi hata cha kuwa shauri waige mfano kutoka katika nchi ya Urusi ambayo ina namba maalum ya kuanza kwa wachezaji wa kigeni.
    blatter_3031222b
    Wazo hilo la Blatter lilizua ugomvi kati yake na Rais wa shirikisho la soka barani Ulaya Michel Platin kabla ya mpango huo kufutwa mwaka 2010, kwani Umoja wa nchi za Ulaya (EU) unaunga mkono mpango uhuru wa kufanya kazi, hata hivyo Urusi haipo ndani ya Umoja wa nchi za Ulaya (EU).
    “Kuwaiga Urusi kwa kudhibiti idadi ya wachezaji wa kigeni wanaoanza katika mechi moja, kuweka idadi ya wachezaji sita au watano ili kulinda vipaji vya wachezaji wa nchi husika, asilimia 77 ni wachezaji wa kigeni waliopata muda wa kucheza zaidi katika Ligi Kuu Uingereza msimu uliopita”
    sepp_blatter_rtr_img
    Hata hivyo Blatter anaunga mkono Urusi kuweka kiwango hicho cha idadi ya wachezaji wazawa kupewa nafasi kubwa ya kuanza katika mechi za Ligi kuu ya Urusi na anaamini mpango wao huo utawapa nafasi ya kufanya vizuri katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 litakalofanyika Urusi.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni