.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Alhamisi, 13 Agosti 2015

Tagged Under:

EDIN DZEKO AKAMILISHA USAJILI WAKE WA MKOPO LEO, ATAMBULISHWA RASMI AS ROMA APEWA JEZI NO.9

By: Unknown On: Alhamisi, Agosti 13, 2015
  • Share The Gag

  • www.bukobasports.com
    Mshambuliaji wa klabu ya Manchester City Edin Dzeko amejiunga na kilabu ya ligi ya Seria A Roma kwa mkopo.
    Kilabu hiyo imetoa kitita cha pauni milioni 2.9, na nyengine pauni 7.9 zikitarajiwa kulipwa iwapo uhamisho huo utabadilika na kuwa wa kudumu.
    ''Nimekuja hapa kushinda mataji'',alisema Dzeko.
    ''Ninaweza kuahidi kitu kimoja kwamba nitajitahidi vilivyo katika kilabu hii''.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na kilabu ya Etihad kutoka Wolfsburg mnamo mwaka 2011 kwa pauni milioni 27.
    Alikuwa ameweka sahihi ya kandarasi ya miaka minne katika uwanja wa Etihad msimu uliopita.
    Hatahivyo,meneja manuel Pelegrini hivi majuzi alikiri kwamba Dzeko alikuwa na uwezo mkubwa kuondoka katika Etihad kufutia usajili wa Raheem Sterling kutoka Liverpool kwa kitita cha pauni milioni 49.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni