Ligi kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga imeanza rasmi leo kwa
mabingwa watetezi wa ligi hiyo FC Bayern Munich kuwakaribisha Hamburg
katika dimba la Alianz Arena.
Wakicheza mchezo wa kuvutia na wa kasi FC Bayern wameibuka na ushindi wa magoli 5-0.
Beki wa Kimorocco Mehd Benatia alianza kuifungia Bayern goli katika
dakika ya 27 ya mchezo kabla ya Robert Lewandoski kuongeza la pili
katika dakika ya 53.
Mshambuliaji
wa kijerumani Thomas Muller alifunga mara mbili ndani ya dakika 4 za
mchezo huo katika kipindi cha pili dakika ya 69 na 72.
Kiungo
mpya wa timu hiyo Douglas Costa alifunga ukurasa wa magoli matano ya
Bayern kwa kufunga goli la kwisho katika dakika ya 87.
Bayern wanakaa kileleni mwa Bundesliga wakiwa na pointi 3 na magoli ya kufunga 5 huku wakiwa hawajaruhusi wavu wao kuguswa.
Jumamosi, 15 Agosti 2015
Tagged Under:
Hivi ndivyo FC Bayern Munich ilivyoanza kwa kishindo kutetea ubingwa wao.
By:
Unknown
On: Jumamosi, Agosti 15, 2015
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 maoni:
Chapisha Maoni