
Ripoti hizo, ambazo chanzo chake ni Wasambaza Habari wa France Le10sport.com, zimedai Kiungo huyo alishaafikiana maslahi yake binafsi na Man United na kilichobaki ni Klabu husika kukubaliana Ada ya Uhamisho.
Kuhusu Pedro, inasemekana Man United na Barcelona tayari wana makubaliano ila Barca wanataka Fowadi huyo abakie kwao hadi wamalize kucheza na Sevilla kwenye Fainali ya UEFA SUPER CUP itakayochezwa Jumanne huko Tbilisi, Georgia.
Klabu hizo mbili zimekubaliana Ada ya Uhamisho ya Pauni Milioni 18.1 ambayo itapanda kwa Pauni Milioni 4.2 kutokana na Bonasi mbalimbali za mafanikio ya Fowadi huyo.
0 maoni:
Chapisha Maoni