KLABU
 ya Chelsea imemsajili Radamel Falcao kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu 
kutoka Monaco, huku kinda wa Blues, Mario Pasalic akihamia kwa wapinzani
 kama sehemu ya makubaliano ya dili hilo.
Mshambuliaji
 huyo wa Colombia atacheza Ligi Kuu ya England kwa msimu wa pili akiwa 
na kikosi cha Jose Mourinho, baada ya kushindwa kung'ara akiwa na 
Manchester United msimu uliopita.
"Nina
 furaha sana kujiunga na Chelsea na nina hamu ya kuanza mazoezi na 
kusaidia dhamira yetu ya kutetea ubingwa na kupata mafaniko Ulaya," 
amesema Falcao.

Kipa wa Chelsea, Thibaut Courtois akiokoa dhidi ya Radamel Falcao msimu uliopita; wawili hao sasa wanaungana London
Mchezaji
 huyo mwenye umri wa miaka 29, aliitua Old Trafford msimu uliopita kama 
mmoja wa washambuliaji tishio Ulaya, lakini maumivu ya goti aliyoyapata 
wakati anacheza Monaco yalionekana kumpunguza makali.
Kinda
 Mcroatia, Pasalic, ambaye msimu uliopita alikuwa kwa mkopo Elche katika
 La Liga, sasa atakwenda kwa mkopo Monaco kama sehemu ya dili hilo.
Falcao
 ataungana na Diego Costa, Thibaut Courtois na Filipe Luis, ambao wote 
wamewahi kuchezea Atletico Madrid, sambamba na mchezaji mwenzake wa 
kimataifa wa Colombia, Juan Cuadrado Uwanja wa Stamford Bridge. 

0 maoni:
Chapisha Maoni