Ligi
kuu Tanzania Bara itaendelea wikiendi hii huku kocha wa mabingwa wa
zamani wa Tanzania Bara, Simba, Mserbia Goran Kopunovic akiipigia
mahesabu ya ushindi timu ya Kagera Sugar katika uwanja wa Uwanja wa CCM
Kambarage Mjini Shinyanga ambao wanautumia kama uwanja wao wa Nyumbani
baada ya ule wa Kaitaba kuwa kwenye Matengenezo. Mchezo huo unatarajiwa
kuchezwa hapo Jumamosi kesho kutwa.
Katika
kile kinachoonekana mpango mzima wa kulipiza kisasi, Kopunovic amesema
wachezaji wake wapo imara kuifunga Kagera Sugar katika uwanja wa
nyumbani. Kagera Sugar ikiwa na pointi 28, ilifanikiwa kuifunga Simba
1-0 katika mchezo wao uliopita.
Simba
ina pointi 32, ikiwa ya tatu katika msimamo, ambapo wapinzani wao wa
jadi, Yanga wanaongoza Ligi wakiwa na pointi 40 huku Azam wakiwa nafasi
ya pili na pointi 36.Mechi nyingine za Jumamosi ni Coastal Union itakapocheza na Tanzania Prisons mkoa wa Tanga, Kaskazini mwa Tanzania.
Alhamisi, 2 Aprili 2015
Tagged Under:
SIMBA YAIPANIA KAGERA SUGAR CCM KAMBARAGE JUMAMOSI.
By:
Unknown
On: Alhamisi, Aprili 02, 2015
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 maoni:
Chapisha Maoni