.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Alhamisi, 2 Aprili 2015

Tagged Under:

COASTAL YAIPIGIA HESABU PRISON, YAWEKA MIPANGO YA KUHAKIKISHA POINTI TATU ZINABAKI MKWAKWANI.

By: Unknown On: Alhamisi, Aprili 02, 2015
  • Share The Gag
  • unnamed
    wachezaji wa Coastal Union wakiwa na
    mazoezi jana kwenye viwanja vya shule ya sekondari Popatlaly chini ya
    Kocha Mkuu Jamhuri Kihwelu “Julio”,
    ………………………………………………….
    NA MWANDISHI WETU, TANGA
    Timu ya Coastal Union ameanza kuzipigia hesabu pointi tatu muhimu za
    wapinzani wao Tanzania Prison ili kuweza kuhakikisha wanazichukua
    wakati watakapokutana kwenye mechi ya Ligi kuu Tanzania bara.
    Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa wikiendi hii kwenye uwanja wa CCM
    Mkwakwani ikiwa ni mzunguko wa pili wa ligi hiyo ikielekea lala
    salama.Akizungumza leo mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu hiyo
    yanayo endelea kwenye viwanja vya shule ya sekondari Popatlaly mjini
    hapa,Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema kikubwa zaidi
    wanachojivunia ni kuendelea kuimarika kikosi hicho.
    Amesema kuwa mipango yake mikubwa ni kuiwezesha timu hiyo kupata
    matokeo mazuri katika mechi zote zilizosalia ikiwemo kuwataka
    wachezaji kutimiza wajibu wao wa kuipa ushindi timu hiyo.
    Amesema kuwa dhamira yao kubwa ni kupambana kufa na kupona ili
    kumaliza ligi hiyo wakiwa nafasi tatu za juu kwenye michuano hiyo
    ambayo msimu huu imeonekana kuwa na upinzani mkubwa.
    Hata hivyo amewataka mashabiki pamoja na wapenzi kujitokeza kwa wingi
    katika michezo yao iliyosalia ikiwemo ya ugenini na nyumbani ili kuipa
    hamasa timu hiyo kufikisha malengo yao.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni