UROPA
LIGI, Mashindano makubwa ya pili kwa Klabu Barani Ulaya, Usiku huu
Alhamisi yamemaliza Mechi zake za Robo Fainali na Mabingwa Watetezi
Sevilla ya Spain, Dnipro Dnipropetrovsk ya Ukraine na Timu mbili za
Italy, Fiorentina na Napoli, zimefuzu kuingia Nusu Fainali. Fiorentina wamefuzu kuingia Nusu Fainali ya EUROPA LIGI baada ya kuitandika Dynamo Kiev Bao 2-0 na kusonga kwa Jumla ya Bao 3-1 katika Mechi mbili.
Dakika 3 baadae Mario Gomes akaipa Fiorentina Bao na wakapiga Bao la Pili Dakika ya 90 kupitia Juan Manuel Vargas.
Napoli wameingia Nusu Fainali ya EUROPA LIGI baada ya kutoka Sare 2-2 na Wolfsburg na kufuzu kwa Jumla ya Mabao 6-3 kufuatia ushindi wao wa 4-1 wa Ugenini huko Germany Wiki iliyopita.
Hadi Mapumziko Bao zilikuwa 0-0 lakini Napoli waliingia Kipindi cha Pili wakiwa moto na kufunga Bao 2 katika Dakika za 50 na 65 kupitia Jose Callejon na Dries Mertens.
Kufuatia Sare ya 0-0 Ugenini, Dnipro wakicheza kwao walishinda 1-0 na kuingia Nusu Fainali ya EUROPA LIGI.
Dnipro walipata Bao lao la ushindi Dakika ya 83 Mfungaji akiwa Yevgeniy Shakhov.
ZENIT 2 vs 2 SEVILLA
Mabingwa Watetezi wa EUROPA LIGI, Sevilla, wakicheza Ugenini huko Urusi, walitoka Sare 2-2 na Zenit lakini wamefuzu kwa Jumla ya 4-3.
Sevilla walipata Bao muhimu Dakika ya 85 kupitia Kevin Gameiro na Gemu kuwa 2-2.
0 maoni:
Chapisha Maoni