Kagera Sugar imeshinda mechi tano Uwanja wa Kambarage tangu ihamishie
maskani yake mjini Shinyanga ikitokea Mwanza ilikopoteza mechi tatu
mfululizo na kulazimika kuhama.’
KAGERA Sugar FC imesahihisha makosa ya kufungwa 2-1 dhidi ya Simba SC
wiki iliyopita baada ya kuilaza Ruvu Shooting Stars mabao 2-0 katika
mechi pekee ya leo ya Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa Uwanja wa CCM
Kambarage mjini Shinyanga.
Kwa matokeo hayo, Kagera Sugar FC inayonolewa na Mganda Jackson Mayanja,
imeendelea kubaki nafasi ya nne katika msimamo wa ligi ikifikisha
pointi 31 baada ya mechi 22, pointi nne nyuma ya Simba SC inayokamata
nafasi ya tatu baada ya mechi 21.
Kikosi cha Mkenya Tom Olaba cha Ruvu Shooting Stars kimeendelea
kubaki nafasi ya nane katika msimamo wa ligi kikiwa na pointi 26 baada
ya mechi 22.
Victor Hangaya amefunga bao la kwanza la Kagera dakika mbili baada ya
kuanza kwa kipindi cha pili kabla ya Atupele Green kuongeza la pili
katika dakika ya 51 na kuihakikishia Kagera Sugar FC ushindi wa tano
Uwanja wa CCM Kambarage msimu huu tangu wahamishie maskani yake mjini
Shinyanga ikitokea Mwanza Januari mwaka huu.
Kagera Sugar FC imelazimika kuishi mithili ya kumbikumbi kwa kuhamaha
msimu huu kutokana na ukarabati wa Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba,
unaofandhiliwa na FIFA.
Katika mechi ya leo kikosi cha Kagera kimemkosa mshambuliaji wake
tegemeo mwenye magoli 10 msimu huu, Rashid Mandawa kutokana na mchezaji
bora huyo wa mwezi Novemba wa ligi hiyo kuwa na kadi tatu za njano.
Jumanne, 14 Aprili 2015
Tagged Under:
Kagera yaitisha Simba nafasi ya tatu Ligi Kuu Bara
By:
Unknown
On: Jumanne, Aprili 14, 2015
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 maoni:
Chapisha Maoni