.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumatano, 18 Machi 2015

Tagged Under:

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: LEO BARCELONA vs MANCHESTER CITY

By: Unknown On: Jumatano, Machi 18, 2015
  • Share The Gag

  • Manchester City wana kibarua kigumu kusonga Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI kwa mara yao ya kwanza kabisa.
    City Jumatano Usiku wapo Nou Camp kurudiana na Barcelona baada ya kuchapwa 2-1 na Barca wakiwa kwao Etihad Wiki 3 zilizopita katika Mechi ya kwanza.
    Kwenye Mechi hiyo ambayo Barca walitawala, City wangekuwa na kazi ngumu zaidi kama si uhodari w Kipa wao Joe Hart kuokoa Penati ya Dakika za Majeruhi ya Lionel Messi.
    Kwa hali za Timu hizi mbili hivi sasa, Barca wako vyema zaidi baada ya kupanda kileleni mwa La Liga kufuatia ushindi wao wa Mechi 16 kati ya 17 zilizopita.
    Kwa City hali hivi sasa ni tete na Jumamosi walipigwa 1-0 na Timu ya mkiani Burnley na kuharibu matumaini yao ya kutetea Taji lao la Ubingwa wa England.
    Hata hivyo, Meneja wa City anaetoka Chile, Manuel Pellegrini, amesisitiza bado wana matumaini ya kuibwaga Barca kwao.
    Lakini hiyo si kazi rahisi hata kidogo ukichukulia fomu ya Barca hivi sasa na ukali wa Fowadi yao ya Mtu 3 ya Lionel Messi, Neymar na Luis Suarez.
    Kwenye Mechi hii Barca itamkosa Majeruhi Sergio Busquets na hivyo Jeremy Mathieu kucheza badala yake na hili litamfanya Javier Mascherano acheze kama Kiungo Mkabaji.
    City itamkosa Fulbeki wake Gael Clichy ambae yupo Kifungoni baada ya kutolewa kwa Kadi Nyekundu katika Mechi ya kwanza.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni