.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumanne, 10 Machi 2015

Tagged Under:

ACACIA BUZWAGI WATOA MISAADA YA MILIONI 11 KWA WATOTO YATIMA SIKU YA WANANWAKE DUNIANI

By: Unknown On: Jumanne, Machi 10, 2015
  • Share The Gag
  • Kaimu meneja Acacia Buzwagi Simon Sanga akikabidhi zawadi.

    Wanawake wa mgodi wa Acacia Buzwagi kupitia mfuko wa maendeleo wa mgodi huo  wameshiriki siku ya wanawake kwa kutoa misaada mbalimbali kwenye vituo viwili vya kulelea watoto yatima wilayani Kahama mkoani Shinyanga.


    Wanawake hao kupitia kwa makamu meneja wa Acacia Buzwagi Simon Sanga wamekabidhi Misaada hiyo katika vituo vya kulelea watoto yatima vya Muvuma kilichopo Nyasubi pamoja na kituo cha Peace Orphanage Center kilichopo mtaa wa Nyihogo.

    Wafanyakazi wa Mgodi wa Buzwagi wakiwa na watoto wakati wa kutolewa kwa zaiwadi hizo.

    Akikabidhi misaada hiyo makamu meneja wa Acacia Buzwagi Simon Sanga amesema wameamua kutoa misaada hiyo kwa kutambua uwepo wa jamii inayozunguka mgodi na kuongeza kuwa wataendelea kushirikiana na jamii ikiwa ni moja ya wajibu wao kuwasadia wananchi.


    Wakipokea misaada hiyo kwa nyakati tofauti viongozi wa vituo hivyo wameshukuru Acacia Buzwagi kwa kutambua uwepo wa watoto yatima ambao wanahitaji misaada toka kwa wananchi na wadau mbalimbali wanaoguswa na makundi yasiyojiweza katika jamii wakiwemo yatima.

    Picha ya Pamoja ya wafanyakazi wa mgodi wa Buzwagi na watoto Yatima.

    Mkurugenzi wa Peace Orphanage Center Halima Hamza akipokea msaada huo amewashukuru wanawake wa Acacia Buzwagi kwa kukumbuka kundi la yatima katika siku ya wanawake na wakaamua kushiriki kwa kutoa misaada na amewaomba waendelee kufanya hivyo.
    Naye mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha kulelea watoto yatima Muvuma Jacquline Pius kwa niaba ya wenzake amewashukuru wanawake wa Acacia Buzwagi kwa kujitoa na kuwakumbuka na amewakaribisha kushiriki katika masuala mengine katika kituo hicho.

    Wafanyakazi wa Buzwagi wakishiriki michezo mbalimbali na watoto hao.
    Misaada iliyotolewa katika vituo hivyo na wanawake wa Acacia kupitia mfuko wa maendeleo wa mgodi huo ni pamoja na Magodoro,Shuka,Vitanda 6,unga,vifaa vya mashuleni,Mafuta ya kula,na sabuni ambavyo vinathamani ya milion11 na nusu.

    Pia kuna picha za chakula cha pamoja cha mchana na watoto hao,,kuna picha pia za michezo mbalimbali ambazo wafanyakazi wa Mgodi wa Acacia walishiriki michezo hiyo na watoto yatima






    0 maoni:

    Chapisha Maoni