.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Alhamisi, 5 Machi 2015

Tagged Under:

MBUNGE WA JIMBO LA KAHAMA JAMES LEMBELI ATUMA SALAM ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA MAAFA YA WATU 42 WALIOKUFA KWA MVUA YA MAWE NA UPEPO WILAYANI KAHAMA NA WAZIRI MKUU ANAZURU ENEO HILO HII LEO

By: Unknown On: Alhamisi, Machi 05, 2015
  • Share The Gag

  • Mbunge wa jimbo la Kahama James Lembeli (kulia) akiwa na waziri mkuu Mizengo Pinda ambaye leo anazuru eneo lililokubwa na tukio hilo.

    Salaam za rambirambi zimeendelea kumiminika kutoka sehemu mbalimbali nchini, kufuatia maafa ya mvua ya mawe yaliyokikumba kijiji cha mwakata wilayani kahama mkoani Shinyanga ambapo watu 42 wamepoteza maisha na wengine 91 kulazwa hospitalini kwa matibabu.

    Mbunge wa jimbo la kahama James Lembeli akiwa safarini kikazi nchini Ethiopia, amempa pole mkuu wa wilaya hiyo Benson Mpesya na Mbunge wa Jimbo la Msalala Ezekiel Maige kwa kufikwa na janga hilo kubwa na la kihistoria wilayani humo.

    Akiwasiliana na Dunia Kiganjani Blog kwa njia ya mtandao Lembeli amesema amepokea taarifa za msiba huo kwa masikitiko makubwa kwa kuwa watu wa mwakata amekuwa nao karibu na wanampenda huku na yeye anawapenda.

    Lembeli amesisitiza, pamoja na kuwa safarini nje ya nchi lakini yuko pamoja na wale wote waliofikwa na maafa hayo; kwa kuwaombea marehemu wapate pumziko la amani na Mwenyezi mungu awarejeshee majeruhi afya yao haraka.

    Wakati huhohuo, Mazishi ya miili ya watu 42 waliopoteza maisha kwenye janga hilo yamefanyika huku kasoro baadhi zikijitokeza.

    Mpesya amesema katika familia moja (jina halikutajwa), iliyopotelewa na watoto watatu wa kike na wawili wa kiume imeghafilika na kuwazika marehemu pamoja, katika makaburi mawili kwa kufuata jinsi ya me na ke.

    Amesema, yeye kama kiongozi ameamru mazishi hayo yafanyike upya kesho asubuhi, kwani mira na desturi za kiafrika zinaelekeza kila mwili unapaswa kuzikwa kwenye kaburi lake; na siyo kuchanganywa na mwili mwingine hata kama ni ndugu.

    Mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na upepo mkali na mafuliko imenyesha usiku wa kumkia leo katika kijiji cha Mwakata kata ya Isaka wilayani Kahama na kusabisha vifo vya watu na mifugo, huku familia zaidi ya 500 zikiachwa bila makazi.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni