Wachezaji wa klabu ya Dar Swim Club wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuondoka.
Na Mwandishi wetu
Kocha
wa klabu ya kuogolea ya Dar Swim Club, Michael Livingstone ametamba kuwa
waogelaji wake chipukizi watatwaa medali mbalimbali katika mashindano
ya kuogelea ya kimataifa ya Dubai yanayojulikana kwa jina la “Hamilton
Aquatics Dubai Long Course” yaliyopangwa kuanza Disemba 11.
Akizungumza
jijini jana, Livingstone alisema kuwa waogeleaji wote 13 wapo katika
morali ya hali ya juu baada ya kupata maandalizi ya miezi miwili.
Livingstone
alisema kuwa mashindano hayo ambayo yanashirikisha waogelaji kutoka
nchi mbalimbali duniani, mbali ya kusaka medali, pia yatawapa uzoefu
wachezaji wao ambao ni bado chipukizi.
Alisema
kuwa mashindano hayo ni makubwa sana katika mchezo huo na hivyo
watatumia fursa ili kuwapa uzoefu wa kimatafa waogelaji wao ambao ni
hazina ya Tanzania katika mashindano ya kimataifa katika miaka ijayo.
“Timu
yetu inaundwa na waogeleaji chipukizi sana, wengi wao chini ya miaka 15,
mbali ya kushindana, pia watakuwa wanapata uzoefu wa kimataifa kwa
ajili ya kuiwakilisha nchi katika mashindano mengine ya kimataifa kama,
Mashindano ya Dunia, Jumuiya ya Madola namichezo ya Olimpiki,” alisema
Livingstone.
Alisema
kuwa waogeleaji wamesema kuwa hakuna cha kuogopa katika mashindano hayo
ambayo yatamalizika Desemba 12, Livingstone, Kocha mwingine wa klabu
hiyo,
Kocha
mwingine wa timu hiyo, Ferick Kalengela alisema kuwa pamoja na kujiandaa
katika katika bwawa la kuogelea la mita 25, wataweza kushindana katika
Bwawa la Mita 50 kwani waliongeza muda na umbali wakati wa mashindano.
Kalengela
alisema kuwa wamejifunza stamina, kasi ya kuogelea na mambo mengine
mengi yanayohusu mashindano hayo na kupata majina ya waogeleaji bora 13.
Katibu
Mkuu wa klabu hiyo, Inviolata Itatiro alisema kuwa maandalizi yote ya
safari hiyo yamekamilika na wanatarajia kuondoka nchini kesho Jumatano
kuelekea kwenye mashindano hayo.
Inviolata
aliwataja waogeleaji hayo kuwa ni Lidia Janik, Deeptti Venugopal, Maia
Tumiotto, Ursula Khimji, Anna-Clara Azzoni, Maya Somaiya and Niki
Somaiya. Also in the list are Smriti Gokarn, Anjani Taylor, Kayla Temba,
Celina Itatiro, Peter Itatiro na Marin de Villard.
Viongozi ni Michael Livingstone na Kanis Mabena ambao ni makocha na Inviolata ambaye ni meneja na mkuu wa msafara.
0 maoni:
Chapisha Maoni