.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Alhamisi, 17 Desemba 2015

Tagged Under:

JOSE MOURINHO ASIMAMISHWA KAZI NA CHELSEA!

By: Unknown On: Alhamisi, Desemba 17, 2015
  • Share The Gag

  • Mmiliki wa klabu ya Chelsea Roman Abramovich alikutana na bodi ya klabu hiyo kujadili hatima ya meneja wa klabu hiyo Jose Mourinho na sasa kuamua kumtimua.
    Hii ni baada ya klabu hiyo kuandikisha matokeo mabaya sana msimu huu, matokeo ya karibuni zaidi yakiwa kuchapwa 2-1 na Leicester ligini Jumatatu.
    Hiyo ilikuwa mara ya tisa kwa Chelsea kushinda Ligi ya Premia katika mechi 16 na sasa wamo alama moja pekee juu ya eneo la kushushwa daraja.

    Mechi inayofuata kwa Chelsea ni Sunderland Jumamosi uwanjani Stamford Bridge.
    Abramovich alitangaza kwamba bado alikuwa akimuunga mkono Mourinho Oktoba lakini matokeo hayajaimarika.
    Abramovich na wenzake uongozini Chelsea wamekuwa wakimuunga mkono meneja huyo lakini kuna kizungumkuti cha matokeo mabaya na kuendelea kufanya vibaya Kwa Klabu hiyo kuimeifanya Imtimue Meneja wake na hii ni baada ya kutoimarika kwa Klabu hiyo.


    Meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola na Diego Simeone Atletico Madrid bado wana majukumu kwa sasa. Hili limepelekea uvumi kwamba sasa huenda Chelsea ikarudi tena kwa Guus Hiddink kwa mkataba wa muda.Jose Mourinho hapa alioneka akiwa na Kikosi cha  Chelsea siku ya Jumanne wakifanya mazoezi na leo hii Alhamisi Kutimliwa.

    Mourinho sasa kuuangalizia Mtanange wa Chelsea dhidi ya Sunderland kwenye Tv

    Mourinho amekuwa kwenye kizungumkuti baada ya Msimu huu Kikosi Chake kutofanya Vyema


    Kipigo cha bao 2-1 kutoka kwa  Leicester jumatatu kiliongeza Machungu kwa Mmiliki na Wapenzi wa Soka wakiwemo Mashabiki wake.

    Mourinho alisukumiza sababu kwa Wachezaji wake kuwa ndio waliosababisha katika Mechi hiyo lakini Mmiliki wa Klabu hiyo Bwana Roman Abramovich aliitisha Kikao na Sasa wameamua kumtimua Kiongozi huyo mwenye Makeke mengi na Majigambo mengi kwenye Soka.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni