
Wakati huo haikujulikana kama aliumia vibaya lakini baada ya kwenda kwa Mtaalam huko kwao Spain ikagundulika kuna kamba ngumu ya Musuli ndani ya Goti imekatika na alipaswa kufanyiwa upasuaji.
Wenger ameeleza: “Santi alitaka amalize tatizo lake haraka ili apone mapema na akaamua kupasuliwa mara moja. Yule Mtaalam alisema ni wazi lipo tatizo hilo na akashauri upasuaji. Santi akakubali moja kwa moja bila kutafuta ushauri mwingine wa Kidaktari ili asicheldewe kupona haraka!”

Wenger amesema kupona kwa Cazorla kutachukua Miezi 3 au 4 ili arejee Uwanjani na si Msimu wote.
Majeruhi wengine wa muda mrefu wa Arsenal ni Mikel Arteta, Danny Welbeck, Tomas Rosicky na Francis Coquelin.
0 maoni:
Chapisha Maoni