.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumapili, 13 Desemba 2015

Tagged Under:

Kumbe Yaya Toure asingekuwa mwanasoka angefanya kazi hii..

By: Unknown On: Jumapili, Desemba 13, 2015
  • Share The Gag


  • Kila mtu ana kipaji chake katika maisha..wapo waliotamani kufanya hivi lakini mwisho wa siku wakajikuta wanafanya kitu kingine kabisa mbacho hawakudhamiria kufanya.
    Kwa mchezaji wa Manchester City na timu ya Taifa ya Ivory Coast Yaya Toure kumbe endapo mambo yasingemnyookea kwenye soka basi angekuwa mcheza karate.
    Huo ndio mchezo ambao kiungo huyo alikuwa ameanza kucheza wakati akiwa bado mdogo na huenda mpaka sasa angebaki kwenye mchezo huo endapo baba yake mzazi asingemkataza akihofia angepata majeraha kupitia mchezo huo.
    Wakati akiwa mdogo katika kipindi cha wiki moja, alifanya vyema na aliweza kuteuliwa kushiriki katika mashindano makubwa yaliyofanyika Kenya ambayo hata hivyo hakwenda kutokana na baba yake kumzuia.
    Kiungo huyo amekuwa na mafanikio makubwa kupitia soka na juzi alifanikiwa kushinda tuzo ya BBC aambayo huyolewa kila mwaka kwa mchezaji bora Afrika.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni