Mechi
ya Robo Fainali ya Kombe kongwe Duniani FA CUP kati ya Timu
zinazoshikilia Rekodi ya kulitwaa mara nyingi kupita wengine, Manchester
United na Arsenal, imethibitishwa kuwa itachezwa Old Trafford Jijini
Mnchester hapo Jumatatu Machi 9 kuanzia Saa 4 Dakika 45 Usiku, Bongo
Taimu.Akiongea mara baada ya Droo ya Mechi hizi za Robo Fainali, Meneja wa Man United Louis van Gaal alisema: “Kitu muhimu ni kupangwa kucheza Nyumbani. Katika Mechi za FA CUP, naamini hilo ni muhimu, kwa hiyo nimefurahishwa tunacheza na Arsenal Nyumbani!”
Mechi nyingine za Robo Fainali ni kati ya Bradford City na Reading, Aston Villa kucheza Dabi ya Midlands na West Bromwich Albion wakati Liverpool wapo kwao Anfield kuivaa Blackburn Rovers.
FA CUP:RATIBA ROBO FAINALI
Jumamosi Machi 7
15:45 Bradford v Reading
20:30 Aston Villa v West Brom
Jumapili Machi 8
19:00 Liverpool v Blackburn
Jumatatu Machi 9
22:45 Man United v Arsenal
TAREHE ZA RAUNDI: -Raundi ya 6 [Robo Fainali]: 7 Machi 2015
-Nusu Fainali: 18 & 19 Aprili 2015
-Fainali: 30 Mei 2015
0 maoni:
Chapisha Maoni