Katika
matukio ya mauaji yaliyotikisa Tanzania hivi karibuni ni pamoja na tukio
la mauaji ya watu wanane Tanga na mengine yaliyofanyika msikitini
mkoani Mwanza.
Leo June 2016 Jeshi la polisi Dar es salaam kupitia kwa Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam, Simon Sirro ametoa taarifa ya kuuwawa kwa majambazi wawili wanaodaiwa kuhusika na matukioa hayo.
Sirro
amesema jeshi hilo limemuua jambazi sugu aliyejulikana kwa jina la
Salum Mhangwa aliyedaiwa kuhusika na mauaji msikitini mkoani Mwanza na
kufanya matukio ya kiuhalifu, jambazi huyo alikutwa na bomu la kurusha
kwa mkono.
Jeshi hilo
pia limemuua jambazi sugu aliyedaiwa kuhusika na mauaji ya watu nane
mkoani Tanga ambaye alikuwa anatumia silaha kali kama bomu la kurusha
kwa mkono na bastola ambavyo alikutwa navyo
0 maoni:
Chapisha Maoni