Argentina Alfajiri ya Jumatatu walipokea kipigo chao
cha tatu cha Fainali kubwa katika Miaka Mitatu baada ya kubwagwa kwa
Penati 4-2 na Chile kwenye Fainali ya Copa America Centenario
iliyochezwa USA.
Mwaka Jana Argentina walibwagwa kwa Penati na Chile
huko Santiago, Chile kwenye Fainali ya Copa America na Mwaka Juzi
walifungwa 1-0 na Germany kwenye Fainali ya Kombe la Dunia huko Brazil.
Akiongea
baada ya Messi kutangaza kustaafu kuichezea Argentina, Aguero alisema:
“Pengine Messi hatakuwa peke yake kuondoka Timu ya Taifa. Wapo Wachezaji
kadhaa wanaotafakari kubaki au kuondoka!”
Alipohojiwa kuhusu
kustaafu kwa Messi, Aguero, mwenye Miaka 28, alisema hajawahi kumuona
mwenzake huyo, ambae amecheza Soka nae tokea utotoni, akiwa amevunjika
moyo kabisa.
Aguero alieleza: “Kwa bahati mbaya, Mtu pekee
alievunjika moyo kiasi kikubwa ni yeye. Sijawahi kumuona hali ile.
Alijaribu kila awezalo kutufikisha hapa!”
0 maoni:
Chapisha Maoni