Michuano ya Euro 2016 imeendelea tena kwa michezo miwili kukamilisha hatua ya 16, mchezo wa Hispania mabingwa watetezi wa Euro walicheza dhidi ya timu ya taifa ya Italia katika mchezo wa hatua ya 16 bora, Hispania ambao walikuwa Mabingwa watetezi wa Euro mara mbili mfululizo kwa kushinda Euro 2008 na 2012.
Hispania wamekubali kipigo cha goli 2-0 kutoka kwa Italia, magoli ambayo yalianza kufungwa dakika ya 33 na Giorgia Chiellin na Graziano Pelle dakika ya 90, baada ya kufungwa goli la kwanza Hispania
ambao wachezaji wake huwa wana asili ya kumiliki mpira walianza
kumiliki mpira kwa kiasi kikubwa, kitendo ambacho hakikuwasaidia.
0 maoni:
Chapisha Maoni