.

.

.

.

.

.

.

,

,

.

.

Jumatatu, 13 Februari 2017

Tagged Under:

RATIBA UEFA CHAMPIONS LEAGUE: JUMANNE NI BENFICA vs BVB, PSG vs BARCELONA, JUMATANO NI BAYERN vs ARSENAL, REAL MADRID vs NAPOLI

By: Unknown On: Jumatatu, Februari 13, 2017
  • Share The Gag

  • UEFA CHAMPIONS LIGI
    Raundi ya Mtoano ya Timu 16 

    Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku
    Mechi za Kwanza
    Jumanne 14 Februari 2017

    Benfica v Borussia Dortmund
    Paris Saint Germain v Barcelona

    Jumatano 15 Februari 2017
    Bayern Munich v Arsenal
    Real Madrid v Napoli

    Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, inaanza Jumanne Usiku kwa Mechi mbili na Jumatano pia zipo Mechi mbili na kuendelea Wiki ijayo, zote zikiwa ni Mechi za Kwanza za Raundi hiyo.
    Jumanne ni huko Portugal wakati Benfica wakiikaribisha BVB Borussia Dortmund na nyingine ni huko Jijini Paris, Paris pale Paris Saint Germain wakicheza na Barcelona.
    Jumatano pia zipo Mechi 2 za Raundi hii ambapo huko Germany ni Bayern Munich na Arsenal na nyingine ni kule Santiago Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain kati ya Real Madrid na Napoli ya Italy.

    Mechi za Kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UCL zitakamilika Wiki ijayo, Jumanne na Jumatano kwa Mechi 4.

    Dondoo Muhimu:
    Benfica v Borussia Dortmund

    Mechi hii itachezwa huko Estádio do Sport Lisboa e Benfica, Lisbon na kuchezeshwa na Refa mzoefu kutoka Italy Nicola Rizzoli.
    Timu hizi zimekutana mara 2 Ulaya na kila moja kushinda mara moja.
    Benfica watatinga kwenye Mechi hii wakiwakosa Andrija Zivkovic, alie Kifungoni, na Majeruhi Lisandro Lopez huku Jonas akiwa kwenye hatihati kucheza kutokana na maumivu.
    Nao BVB watawakosa Majeruhi Mario Götze na Sven Bender huku hatihati ikiwa kwenye maumivu Nuri Şahin na Sebastian Rode.

    Paris Saint Germain v Barcelona
    Mechi hii ipo ndani ya Parc des Princes Jijini Paris Nchini France na itachezeshwa na Refa Szymon Marciniak kutoka Poland.

    Katika Mechi zilizopita, PSG ilishinda mara 2, Sare 3 na Barca kushinda 4 kati yao.

    PSG kwenye Mechi hii itamkosa Thiago Motta ambaye yupo Kifungoni wakati Barca watawakosa Majeruhi Arda Turan, Javier Mascherano na Aleix Vidal.

    UEFA CHAMPIONS LIGI
    Raundi ya Mtoano ya Timu 16

    Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku 
    Mechi za Kwanza
    Jumanne 21 Februari 2017

    Bayer 04 Leverkusen v Atlético Madrid
    Manchester City v Monaco

    Jumatano 22 Februari 2017
    FC Porto v Juventus
    Sevilla v Leicester City
     

    Mechi za Pili
    Jumanne 7 Machi 2017

    Arsenal v Bayern Munich
    Napoli v Real Madrid

    Jumatano 8 Machi 2017

    Barcelona v Paris Saint Germain
    Borussia Dortmund v Benfica


    Jumanne 14 Machi 2017
    Juventus v FC Porto
    Leicester City v Sevilla

    Jumatano 15 Machi 2017
    Atlético Madrid v Bayer 04 Leverkusen
    Monaco v Manchester City

    0 maoni:

    Chapisha Maoni